-
2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.
-
-
Isaya 42:24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Ni nani aliyemtia Yakobo mikononi mwa watekaji nyara
Na Israeli mikononi mwa waporaji?
Je, si Yehova, Yule ambaye tumemtendea dhambi?
-
-
Yeremia 40:2, 3Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
2 Kisha mkuu wa walinzi akamchukua Yeremia na kumwambia: “Yehova Mungu wako alitabiri msiba huu dhidi ya mahali hapa, 3 na Yehova ameuleta msiba huo kama alivyosema, kwa sababu ninyi watu mlimtendea dhambi Yehova na hamkuitii sauti yake. Ndiyo sababu jambo hili limewapata.+
-