-
Kumbukumbu la Torati 6:10-12Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
10 “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi aliyowaapia mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atawapa ninyi+—majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo hamkujenga,+ 11 nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina mbalimbali ambavyo hamkufanya kazi ili kuvipata, visima ambavyo hamkuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamkupanda—nanyi mtakapokuwa mmekula na kushiba,+ 12 jihadharini msimsahau Yehova,+ aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.
-
-
Ayubu 31:24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Ikiwa nilifanya dhahabu kuwa tumaini langu
Au kuiambia dhahabu bora, ‘Wewe ni mlinzi wangu!’+
-
-
Ayubu 31:28Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
28 Basi hilo ni kosa linalostahili adhabu kutoka kwa waamuzi,
Kwa maana nitakuwa nimemkana Mungu wa kweli aliye juu.
-