-
Ayubu 38:8-10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
8 Na ni nani aliyeizuia bahari nyuma ya milango+
Ilipotoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,
9 Nilipoivalisha mawingu
Na kuifunika kwa* giza zito,
10 Nilipoiwekea mpaka wangu
Na kuweka makomeo yake na milango yake mahali pake,+
-
Zaburi 33:7Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+
Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.
-
-
Methali 8:29Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
29 Alipoiwekea bahari sheria
Kwamba maji yake yasipite agizo lake,+
Alipoiweka* misingi ya dunia,
-
Yeremia 5:22Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
22 ‘Je, hamniogopi mimi?’ asema Yehova,
‘Je, hampaswi kutetemeka mbele zangu?
Mimi ndiye niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari,
Sheria inayodumu isiyoweza kukiukwa na bahari.
Ingawa mawimbi yake yanasukasuka, hayawezi kushinda;
Ingawa yananguruma, bado hayawezi kuvuka.+
-
-
-
-
-