-
Kutoka 30:34-36Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
34 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Chukua vipimo vinavyolingana vya manukato haya:+ matone ya natafi, shekelethi, kelbena yenye manukato, na ubani safi. 35 Yatumie kutengeneza uvumba;+ viungo hivyo vinapaswa kuchanganywa kwa ustadi,* vitiwe chumvi,+ viwe safi, na vitakatifu. 36 Utaponda baadhi ya viungo hivyo viwe unga laini na kuweka kiasi fulani mbele ya sanduku la Ushahidi katika hema la mkutano, mahali nitakapokutokea. Mchanganyiko huo unapaswa kuwa mtakatifu kabisa kwenu.
-