-
Marko 15:24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Nao wakamtundika kwenye mti na wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura ili kuamua ni nini ambacho kila mtu angechukua.+
-
-
Luka 23:34Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
34 Lakini Yesu alikuwa akisema: “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui wanachofanya.” Isitoshe, wakapiga kura ili wagawane mavazi yake.+
-
-
Yohana 19:23, 24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
23 Baada ya wanajeshi kumtundika Yesu kwenye mti, wakachukua mavazi yake ya nje na kuyagawanya vipande vinne, kila askari kipande kimoja, na pia wakachukua vazi la ndani. Lakini vazi la ndani halikuwa na mshono, lilikuwa limefumwa kutoka juu mpaka chini. 24 Basi wakaambiana: “Tusilirarue, badala yake tupige kura ili tuamue litakuwa la nani.”+ Hilo lilitimiza andiko linalosema: “Waligawana mavazi yangu, na wakalipigia kura vazi langu.”+ Kwa kweli, hivyo ndivyo walivyofanya wale wanajeshi.
-