-
2 Wafalme 5:20-22Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
20 Gehazi+ mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu wa kweli+ akasema moyoni mwake: ‘Tazama, Bwana wangu amemwacha huyu Naamani Msiria+ aende zake kwa kukataa kupokea vitu alivyoleta. Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, nitakimbia na kumfuata, nichukue kitu fulani kutoka kwake.’ 21 Kwa hiyo Gehazi akamfuata mbio Naamani. Naamani alipoona mtu fulani akimfuata mbio, akashuka kutoka kwenye gari lake na kwenda kumpokea, akamuuliza: “Je, mambo yote yako sawa?” 22 Akasema: “Mambo yote yako sawa. Bwana wangu amenituma nikwambie, ‘Tazama! Sasa hivi vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamekuja kwangu kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu. Tafadhali, wape talanta moja ya fedha na mavazi mawili.’”+
-