-
2 Wafalme 16:8, 9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
8 Kisha Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* akampelekea mfalme wa Ashuru kama rushwa.+ 9 Mfalme wa Ashuru akakubali ombi lake, naye akapanda kwenda Damasko na kuliteka jiji hilo na kuwapeleka watu wake uhamishoni huko Kiri,+ akamuua Resini.+
-
-
Isaya 8:4Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
4 kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita, ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mali za Damasko na nyara za Samaria zitachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.”+
-