-
Yeremia 32:17-19Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
17 “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama! Uliumba mbingu na dunia kwa nguvu zako kuu+ na kwa mkono wako ulionyooshwa. Hakuna jambo la ajabu sana kwako, 18 Wewe unayewatendea kwa upendo mshikamanifu maelfu ya watu, lakini unawaadhibu wana kwa sababu ya makosa ya baba zao,+ Mungu wa kweli, uliye mkuu na Mwenye nguvu, ambaye jina lako ni Yehova wa majeshi. 19 Wewe ni mkuu katika kutoa mashauri* na matendo yako ni yenye nguvu,+ wewe ambaye macho yako huchunguza njia zote za wanadamu,+ ili kumlipa kila mtu kulingana na njia zake na matendo yake.+
-