-
Mathayo 13:39Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
39 na adui aliyepanda magugu ni Ibilisi. Mavuno ni umalizio wa mfumo wa mambo,* na wavunaji ni malaika.
-
-
Marko 13:3, 4Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
3 Alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, huku hekalu likiwa linaonekana, Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea wakamuuliza faraghani: 4 “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, na nini itakayokuwa ishara ya wakati ambapo mambo haya yatafikia mwisho?”+
-
-
Luka 21:7Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
7 Ndipo wakamuuliza: “Mwalimu, kwa kweli mambo haya yatatukia lini, na ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya yanakaribia kutokea?”+
-