Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Danieli 9:27
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 27 “Naye atalitendesha agano kwa ajili ya wengi kwa juma moja; na katika nusu ya juma hilo atakomesha dhabihu na toleo la zawadi.+

      “Na juu ya bawa la vitu vyenye kuchukiza sana kutakuwa na yule anayesababisha ukiwa;+ na mpaka wakati wa maangamizi, kilichoamuliwa kitamwagwa pia juu ya yule anayekaa ukiwa.”

  • Danieli 11:31
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 31 Na majeshi yatasimama, kutoka kwake; nayo yatachafua patakatifu,+ ile ngome, na kuondoa ile dhabihu inayotolewa daima.*+

      “Nao watasimamisha kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa.+

  • Danieli 12:11
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 11 “Na tangu wakati wa kuondolewa kwa ile dhabihu inayotolewa daima*+ na kusimamishwa kwa kile kitu kinachochukiza sana kinachosababisha ukiwa,+ kutakuwa na siku 1,290.

  • Marko 13:14-18
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 14 “Hata hivyo, mtakapoona kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa+ kikiwa kimesimama mahali ambapo hakipaswi kuwa (msomaji na atumie utambuzi), ndipo wale walio Yudea waanze kukimbilia milimani.+ 15 Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke wala asiingie kuchukua kitu chochote ndani ya nyumba yake; 16 na mtu aliye shambani asirudi kwenye vitu vilivyo nyuma ili kuchukua vazi lake la nje. 17 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto katika siku hizo!+ 18 Endeleeni kusali kwamba isitukie wakati wa majira ya baridi kali;

  • Luka 21:20
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki