-
Danieli 9:27Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
27 “Naye atalitendesha agano kwa ajili ya wengi kwa juma moja; na katika nusu ya juma hilo atakomesha dhabihu na toleo la zawadi.+
“Na juu ya bawa la vitu vyenye kuchukiza sana kutakuwa na yule anayesababisha ukiwa;+ na mpaka wakati wa maangamizi, kilichoamuliwa kitamwagwa pia juu ya yule anayekaa ukiwa.”
-
-
Marko 13:14-18Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
14 “Hata hivyo, mtakapoona kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa+ kikiwa kimesimama mahali ambapo hakipaswi kuwa (msomaji na atumie utambuzi), ndipo wale walio Yudea waanze kukimbilia milimani.+ 15 Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke wala asiingie kuchukua kitu chochote ndani ya nyumba yake; 16 na mtu aliye shambani asirudi kwenye vitu vilivyo nyuma ili kuchukua vazi lake la nje. 17 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto katika siku hizo!+ 18 Endeleeni kusali kwamba isitukie wakati wa majira ya baridi kali;
-