Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 14:3-9
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 3 Alipokuwa Bethania akila* katika nyumba ya Simoni mwenye ukoma, mwanamke fulani akaja na chupa ya alabasta iliyokuwa na mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana. Akaifungua na kuanza kuyamimina juu ya kichwa cha Yesu.+ 4 Ndipo baadhi yao wakakasirika na kuambiana: “Kwa nini mafuta haya ya marashi yapotezwe bure? 5 Kwa maana mafuta haya yangeuzwa kwa zaidi ya dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo!” Nao wakamkasirikia* sana mwanamke huyo. 6 Lakini Yesu akawaambia: “Mwacheni. Kwa nini mnataka kumsumbua? Amenitendea jambo jema.+ 7 Kwa maana maskini mnao sikuzote,+ na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka, lakini mimi hamtakuwa nami sikuzote.+ 8 Amefanya alichoweza; ameupaka mwili wangu mafuta yenye marashi ili kuutayarisha kwa ajili ya mazishi.+ 9 Kwa kweli ninawaambia, popote ambapo habari njema itahubiriwa ulimwenguni,+ jambo alilofanya mwanamke huyu litatajwa ili kumkumbuka.”+

  • Yohana 12:1-8
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 12 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu akafika Bethania, alikoishi Lazaro+ ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka kwa wafu. 2 Basi, wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha alikuwa akiwahudumia,+ lakini Lazaro alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakila* pamoja na Yesu. 3 Kisha Maria akachukua ratili* moja ya mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana, akammiminia Yesu miguuni na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi.+ 4 Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake aliyekuwa karibu kumsaliti akasema: 5 “Kwa nini mafuta haya yenye marashi hayangeuzwa kwa dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo?” 6 Hakusema hivyo kwa sababu aliwahangaikia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi, naye ndiye aliyetunza sanduku la pesa na alikuwa akiiba pesa zilizowekwa humo. 7 Kisha Yesu akawaambia: “Mwacheni afanye hivyo kwa ajili ya matayarisho ya siku ya mazishi yangu.+ 8 Kwa maana maskini mnao sikuzote,+ lakini mimi hamtakuwa nami sikuzote.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki