-
Marko 14:37-42Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
37 Aliporudi akawakuta wakiwa wamelala usingizi, akamwuliza Petro: “Simoni, unalala? Hukuwa na nguvu za kukesha hata kwa saa moja?+ 38 Endeleeni kukesha na kusali bila kuacha, ili msiingie katika majaribu.+ Bila shaka, roho inataka,* lakini mwili ni dhaifu.”+ 39 Naye akaenda zake tena, akasali, akirudia maneno yaleyale.+ 40 Akaja tena na kuwakuta wakiwa wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa yamelemewa, nao hawakujua la kumjibu. 41 Akarudi mara ya tatu akawaambia: “Mnalala na kupumzika wakati kama huu! Imetosha! Saa imefika!+ Tazama! Mwana wa binadamu anasalitiwa mikononi mwa watenda dhambi. 42 Simameni twende. Tazama! Msaliti wangu amekaribia.”+
-
-
Luka 22:45Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
45 Baada ya kusali, akawaendea wanafunzi, akawakuta wakiwa wamelala usingizi, wakiwa wamechoka kwa sababu ya huzuni.+
-