-
Marko 14:60-65Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
60 Kisha kuhani mkuu akasimama katikati yao, akamuuliza Yesu: “Kwa nini hujibu? Watu hawa wanashuhudia nini kukuhusu?”+ 61 Lakini akakaa kimya na hakujibu.+ Tena kuhani mkuu akaanza kumuuliza: “Je, wewe ndiye Kristo Mwana wa Yule Mbarikiwa?” 62 Ndipo Yesu akasema: “Mimi ndiye; nanyi mtamwona Mwana wa binadamu+ akiwa ameketi kwenye mkono wa kuume+ wa nguvu, akija pamoja na mawingu ya mbinguni.”+ 63 Ndipo kuhani mkuu akayararua mavazi yake na kusema: “Tunahitaji mashahidi wengine wa nini?+ 64 Mmemsikia akikufuru. Uamuzi wenu ni nini?”* Wote wakaamua kwamba anastahili kufa.+ 65 Wengine wakaanza kumtemea mate,+ wakamfunika uso, wakampiga ngumi na kumwambia: “Toa unabii!” Walinzi wa mahakama wakampiga makofi usoni na kumchukua.+
-