-
Luka 18:35-43Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
35 Yesu alipokaribia Yeriko kipofu mmoja alikuwa ameketi kando ya barabara akiombaomba.+ 36 Aliposikia umati ukipita, akaanza kuuliza kilichokuwa kikiendelea. 37 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti ndiye anayepita!” 38 Ndipo akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 39 Wale waliokuwa mbele wakaanza kumkemea wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 40 Kisha Yesu akasimama na kuagiza mtu huyo aletwe kwake. Alipokaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, naomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamwambia: “Ona tena; imani yako imekuponya.”+ 43 Mara moja akaanza kuona tena, naye akaanza kumfuata Yesu+ huku akimtukuza Mungu. Pia, watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.+
-