3 Kuna mtu anayepaza sauti nyikani:
“Fungueni njia ya Yehova!+
Tengenezeni barabara kuu iliyonyooka+ inayopitia jangwani kwa ajili ya Mungu wetu.+
4 Kila bonde na liinuliwe,
Na kila mlima na kilima kishushwe.
Na ardhi yenye mashimo-mashimo itasawazishwa,
Na ardhi yenye mawemawe itakuwa bonde tambarare.+
5 Utukufu wa Yehova utafunuliwa,+
Na wote wenye mwili watauona pamoja,+
Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.”