-
Mathayo 12:1-8Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
12 Wakati huo, Yesu alipitia katikati ya mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake wakahisi njaa wakaanza kukata masuke ya nafaka na kula.+ 2 Mafarisayo walipoona hilo, wakamwambia: “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato.”+ 3 Yesu akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, nao wakala mikate ya toleo,*+ kitu ambacho hakikuwa halali kwake au kwa wale waliokuwa pamoja naye kula, ila makuhani tu?+ 5 Au, je, hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja Sabato na wanabaki bila hatia?+ 6 Lakini ninawaambia, hapa pana mtu mkuu kuliko hekalu.+ 7 Hata hivyo, kama mngeelewa maana ya maneno haya, ‘Ninataka rehema+ si dhabihu,’+ hamngewalaumu watu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa Sabato.”+
-
-
Marko 2:23-28Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
23 Alipokuwa akipita kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato, wanafunzi wake wakaanza kukata masuke ya nafaka huku wakitembea.+ 24 Hivyo, Mafarisayo wakamwambia: “Tazama sasa! Kwa nini wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?” 25 Lakini akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi, wakati alipokuwa na uhitaji na yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 26 Jinsi katika simulizi kuhusu mkuu wa makuhani Abiathari,+ Daudi alivyoingia katika nyumba ya Mungu na kula mikate ya toleo,* ambayo si halali kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani,+ naye akawapa pia watu waliokuwa pamoja naye?” 27 Kisha akawaambia: “Sabato iliwekwa kwa ajili ya mwanadamu,+ bali si mwanadamu kwa ajili ya Sabato. 28 Basi, Mwana wa binadamu pia ndiye Bwana wa Sabato.”+
-