-
Mambo ya Walawi 24:5-9Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
5 “Utachukua unga laini na kuoka mikate 12 ya mviringo. Utatumia sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa* cha unga laini kuoka kila mkate. 6 Utaipanga mikate hiyo kwenye safu* mbili juu ya meza ya dhahabu safi mbele za Yehova,+ kila safu itakuwa na mikate sita.+ 7 Unapaswa kuweka ubani safi juu ya kila safu, na mikate hiyo itakuwa dhabihu ya kumbukumbu*+ inayochomwa kwa moto mbele za Yehova. 8 Kila siku ya Sabato, anapaswa kupanga mikate hiyo mbele za Yehova kwa ukawaida.+ Ni agano linalodumu kati yangu na Waisraeli. 9 Itakuwa ya Haruni na wanawe,+ nao wataila mahali patakatifu,+ kwa sababu ni kitu kitakatifu kabisa kwa ajili ya kuhani kutoka kwa dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto; itakuwa sheria ya kudumu.”
-