-
Mathayo 7:24-27Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 “Kwa hiyo, kila mtu anayesikia haya maneno yangu na kuyatenda ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.+ 25 Kisha mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, upepo ukavuma na kuipiga nyumba hiyo, lakini haikuporomoka, kwa maana msingi wake ulikuwa umejengwa kwenye mwamba. 26 Zaidi ya hayo, kila mtu anayesikia haya maneno yangu lakini hayatendi ni kama mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba juu ya mchanga.+ 27 Kisha mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, upepo ukavuma na kuipiga nyumba hiyo,+ nayo ikaporomoka na kuharibika kabisa.”
-