-
Luka 14:10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
10 Lakini unapoalikwa, nenda uketi mahali pa chini kabisa, ili mtu aliyekualika akija akuambie, ‘Rafiki yangu, nenda uketi mahali pa heshima zaidi.’ Kisha utakuwa na heshima mbele ya wageni wenzako wote.+
-
-
Luka 22:24-26Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Hata hivyo, pia kukatokea bishano kali kuhusu ni nani aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 25 Lakini akawaambia: “Wafalme wa mataifa hupiga ubwana juu yao, na wale walio na mamlaka juu yao huitwa Wafadhili.+ 26 Hata hivyo, ninyi hampaswi kuwa hivyo.+ Lakini yule aliye mkuu zaidi kati yenu anapaswa kuwa mdogo zaidi,+ na yule anayeongoza awe kama anayehudumu.
-