5 Basi Mungu anayetoa uvumilivu na faraja na awawezeshe ninyi miongoni mwenu wenyewe kuwa na mtazamo uleule wa akili ambao Kristo Yesu alikuwa nao, 6 ili kwa umoja+ na kwa sauti moja* mumtukuze Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo.
10 Sasa ninawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mseme kwa upatano, na kwamba kusiwe na migawanyiko kati yenu,+ bali kwamba muunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.+
11 Mwishowe, akina ndugu, endeleeni kushangilia, kurekebishwa upya, kufarijiwa,+ kufikiri kwa upatano,+ kuishi kwa amani;+ na Mungu wa upendo na amani+ atakuwa pamoja nanyi.