-
Matendo 2:29-32Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
29 “Wanaume, akina ndugu, inaruhusika nizungumze nanyi kwa uhuru wa kusema kumhusu Daudi kichwa cha familia, kwamba alikufa, akazikwa,+ na kaburi lake liko hapa kwetu mpaka leo. 30 Kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemwapia kwa kiapo kwamba angemfanya mmoja wa wazao wake* aketi kwenye kiti chake cha ufalme,+ 31 aliona mapema na kusema kuhusu ufufuo wa Kristo, kwamba hakuachwa katika Kaburi* wala mwili wake haukuona uharibifu.*+ 32 Mungu alimfufua, Yesu huyu, na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.+
-