-
Kutoka 12:21-23Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
21 Musa akawaita wazee wote wa Israeli+ bila kukawia na kuwaambia: “Nendeni mkachague wanyama wachanga* kwa ajili ya kila moja ya familia zenu, nanyi mchinje dhabihu ya Pasaka. 22 Kisha mtachovya tita la majani ya hisopo katika damu iliyo ndani ya beseni na kupiga kizingiti cha juu cha mlango na miimo yake miwili kwa tita hilo lenye damu; na mtu yeyote kati yenu asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi. 23 Kisha Yehova atakapopita ili kuwapiga Wamisri na kuiona damu kwenye kizingiti cha juu cha mlango na kwenye miimo yake miwili, kwa hakika Yehova atapita juu ya mlango wenu, naye hataruhusu pigo la kifo liingie* katika nyumba zenu.+
-