-
1 Wafalme 17:22-24Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
22 Yehova akasikiliza ombi la Eliya,+ na uhai wa mtoto huyo ukamrudia, akawa hai tena.+ 23 Eliya akamchukua mtoto huyo, akamleta chini kutoka katika kile chumba cha darini, akampa mama yake; Eliya akasema: “Tazama, mwana wako yuko hai.”+ 24 Ndipo mwanamke huyo akamwambia Eliya: “Sasa ninajua kwamba kwa kweli wewe ni mtu wa Mungu+ na kwamba neno la Yehova kutoka kinywani mwako ni kweli.”
-
-
2 Wafalme 4:32Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+
-
-
2 Wafalme 4:34Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+
-