-
Ezekieli 1:5-10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
5 Katikati yake kulikuwa na mfano wa viumbe hai wanne,+ na kila mmoja wao alifanana na mwanadamu. 6 Kila mmoja wao alikuwa na nyuso nne na mabawa manne.+ 7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, na nyayo za miguu yao zilikuwa kama nyayo za ndama, nayo ilikuwa iking’aa kama shaba iliyong’arishwa.+ 8 Walikuwa na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao pande zote nne, na wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa. 9 Mabawa yao yaligusana. Hawakugeuka walipokuwa wakienda; kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+
10 Nyuso zao zilionekana hivi: Kila mmoja wa viumbe hao wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na uso wa simba+ upande wa kulia, na uso wa ng’ombe dume+ upande wa kushoto, na kila mmoja wa viumbe hao wanne alikuwa na uso+ wa tai.+
-