Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Jibu la Ayubu (1-30)

        • Adai kwamba ana sababu ya kulia (2-6)

        • Wafariji wake ni wenye hila (15-18)

        • “Maneno ya unyoofu hayaumizi!” (25)

Ayubu 6:2

Marejeo

  • +Zb 31:9

Ayubu 6:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nimezungumza bila kufikiri; harakaharaka.”

Marejeo

  • +Mhu 7:7; Yak 3:2

Ayubu 6:4

Marejeo

  • +Met 18:14

Ayubu 6:5

Marejeo

  • +Ayu 24:5

Ayubu 6:9

Marejeo

  • +Hes 11:11, 15; 1Fa 19:3, 4; Yon 4:3

Ayubu 6:10

Marejeo

  • +Law 19:2; Ho. 11:9

Ayubu 6:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hivi kwamba nirefushe maisha yangu (nafsi yangu)?”

Marejeo

  • +Ayu 7:6, 7; Zb 103:15, 16

Ayubu 6:14

Marejeo

  • +Met 3:3; 19:22; Ho. 6:6; Zek 7:9
  • +1Yo 3:17

Ayubu 6:15

Marejeo

  • +Ayu 19:19; Zb 38:11

Ayubu 6:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Msafara wa Wasabea.”

Marejeo

  • +Isa 21:13, 14
  • +Ayu 1:14, 15

Ayubu 6:21

Marejeo

  • +Ayu 13:4
  • +Zb 38:11

Ayubu 6:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nikombolewe.”

Ayubu 6:24

Marejeo

  • +Ayu 32:11, 12

Ayubu 6:25

Marejeo

  • +Met 12:18; 25:11
  • +Ayu 16:2, 3; 21:34

Ayubu 6:26

Marejeo

  • +Ayu 10:1

Ayubu 6:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kubadilishana rafiki yenu kwa mali.”

Marejeo

  • +Ayu 31:21, 22; Mal 3:5
  • +Mwa 37:28

Ayubu 6:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kaakaa langu halitambui.”

Jumla

Ayu. 6:2Zb 31:9
Ayu. 6:3Mhu 7:7; Yak 3:2
Ayu. 6:4Met 18:14
Ayu. 6:5Ayu 24:5
Ayu. 6:9Hes 11:11, 15; 1Fa 19:3, 4; Yon 4:3
Ayu. 6:10Law 19:2; Ho. 11:9
Ayu. 6:11Ayu 7:6, 7; Zb 103:15, 16
Ayu. 6:14Met 3:3; 19:22; Ho. 6:6; Zek 7:9
Ayu. 6:141Yo 3:17
Ayu. 6:15Ayu 19:19; Zb 38:11
Ayu. 6:19Isa 21:13, 14
Ayu. 6:19Ayu 1:14, 15
Ayu. 6:21Ayu 13:4
Ayu. 6:21Zb 38:11
Ayu. 6:24Ayu 32:11, 12
Ayu. 6:25Met 12:18; 25:11
Ayu. 6:25Ayu 16:2, 3; 21:34
Ayu. 6:26Ayu 10:1
Ayu. 6:27Ayu 31:21, 22; Mal 3:5
Ayu. 6:27Mwa 37:28
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 6:1-30

Ayubu

6 Kisha Ayubu akajibu:

2 “Laiti maumivu yangu makali+ yangepimwa kikamili

Na kuwekwa kwenye mizani pamoja na msiba wangu!

 3 Kwa maana sasa ni mazito kuliko mchanga wa bahari.

Ndiyo sababu maneno yangu yamekuwa mazungumzo ya ovyoovyo.*+

 4 Kwa maana mishale ya Mweza-Yote imenichoma,

Na roho yangu inakunywa sumu yake;+

Vitisho vya Mungu vinaniandama.

 5 Je, punda mwitu+ atalia akiwa na majani,

Au ng’ombe dume atalia akiwa na chakula?

 6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi,

Au maji ya mholi yana ladha?

 7 Nimekataa kugusa vitu vya aina hiyo.

Ni kama uchafu katika chakula changu.

 8 Laiti ombi langu lingejibiwa

Na laiti Mungu angenipa ninachotamani!

 9 Kwamba Mungu angekuwa tayari kunipondaponda,

Na kwamba angeunyoosha mkono wake na kuniangamiza!+

10 Kwa maana hata hilo lingenifariji;

Ningeruka kwa shangwe licha ya maumivu yangu yasiyokwisha,

Kwa maana sijayakana maneno ya Aliye Mtakatifu.+

11 Je, nina nguvu za kuendelea kungoja?+

Na ni mwisho gani unaonisubiri, hivi kwamba niendelee kuishi?*

12 Je, nguvu zangu ni kama za mwamba?

Au mwili wangu umetengenezwa kwa shaba?

13 Je, kuna njia yoyote ninayoweza kujisaidia mwenyewe

Wakati nimenyang’anywa njia zangu zote za kujitegemeza?

14 Yeyote anayekataa kumtendea mwanadamu mwenzake kwa upendo mshikamanifu+

Ataacha kumwogopa Mweza-Yote.+

15 Ndugu zangu wenyewe wamekuwa na hila+ kama kijito cha majira ya baridi kali,

Kama maji ya vijito vya majira ya baridi kali yanayokauka.

16 Vimekuwa vyeusi kwa sababu ya barafu,

Na theluji inayoyeyuka imejificha ndani yake.

17 Lakini katika majira ya kiangazi vinakauka na kutoweka;

Joto linapoongezeka, vinakauka.

18 Mikondo yake hugeuka;

Navyo huelekea jangwani na kutoweka.

19 Misafara ya Tema+ huvitafuta;

Wasafiri kutoka Sheba*+ huvingojea.

20 Wameaibika kwa sababu hawakupata walichotumaini;

Wanafika hapo na kukata tamaa tu.

21 Hivyo ndivyo mlivyo kwangu mimi;+

Mmeona mateso ya msiba wangu, nanyi mnaogopa.+

22 Je, nimewaambia, ‘Nipeni kitu fulani,’

Au kuwaomba zawadi yoyote kutoka katika mali zenu?

23 Je, nimeomba niokolewe kutoka mikononi mwa adui

Au niokolewe* kutoka kwa wakandamizaji?

24 Nifundisheni, nami nitanyamaza;+

Nisaidieni kuelewa kosa langu.

25 Maneno ya unyoofu hayaumizi!+

Lakini karipio lenu lina faida gani?+

26 Je, mnapanga njama ya kukosoa maneno yangu,

Maneno ya mtu aliyekata tamaa,+ yanayopeperushwa mbali na upepo?

27 Ninyi hata mngeweza kupiga kura kwa ajili ya yatima+

Na kumuuza rafiki yenu!*+

28 Basi sasa geukeni mnitazame,

Kwa maana siwezi kusema uwongo mbele yenu.

29 Fikirieni tena, tafadhali—msinielewe vibaya—

Naam, fikirieni tena, kwa maana mimi bado ni mwadilifu.

30 Je, ulimi wangu unasema jambo lisilo la haki?

Je, mdomo wangu hautambui* kwamba kuna jambo ambalo si sawa?

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki