Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 16
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mathayo—Yaliyomo

      • Waomba ishara (1-4)

      • Chachu ya Mafarisayo na Masadukayo (5-12)

      • Funguo za Ufalme (13-20)

        • Kutaniko lajengwa juu ya mwamba (18)

      • Kifo cha Yesu chatabiriwa (21-23)

      • Wanafunzi wa kweli (24-28)

Mathayo 16:1

Marejeo

  • +Mt 12:38; Mk 8:11; Lu 11:16

Mathayo 16:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kisicho na uaminifu.”

Marejeo

  • +Mk 8:12
  • +Yon 1:17; Mt 12:39; Lu 11:29

Mathayo 16:5

Marejeo

  • +Mk 8:13-21

Mathayo 16:6

Marejeo

  • +Mk 8:15; Lu 12:1

Mathayo 16:9

Marejeo

  • +Mt 14:17

Mathayo 16:10

Marejeo

  • +Mt 15:34

Mathayo 16:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hamira.”

Marejeo

  • +Lu 12:1

Mathayo 16:13

Marejeo

  • +Mk 8:27-29; Lu 9:18-20

Mathayo 16:14

Marejeo

  • +Mt 14:1, 2
  • +Yoh 1:25, 26

Mathayo 16:16

Marejeo

  • +Mk 8:29; Lu 9:20; Yoh 1:40, 41; 4:25; 11:27
  • +Zb 2:7; Mt 14:33; Mdo 9:20, 22; Ebr 1:2; 1Yo 4:15

Mathayo 16:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa sababu mwanadamu hakukufunulia.”

Marejeo

  • +Mt 11:27

Mathayo 16:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Yoh 1:42
  • +Ro 9:33; 1Ko 3:11; 10:4; Efe 2:20; 1Pe 2:6-8

Mathayo 16:20

Marejeo

  • +Mk 8:29, 30; Lu 9:20, 21

Mathayo 16:21

Marejeo

  • +Zb 16:10; Isa 53:12; Mt 17:22, 23; 20:18, 19; Mk 8:31; Lu 9:22; 24:46; 1Ko 15:3, 4

Mathayo 16:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jitendee kwa fadhili.”

Marejeo

  • +Mk 8:32

Mathayo 16:23

Marejeo

  • +Mk 8:33

Mathayo 16:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi, “Mti wa mateso.”

Marejeo

  • +Mt 10:38; Mk 8:34; Lu 9:23; 14:27

Mathayo 16:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yake.”

  • *

    Au “nafsi yake.”

Marejeo

  • +Mk 8:35; Lu 9:24; 17:33; Yoh 12:25; Ufu 12:11

Mathayo 16:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yake.”

  • *

    Au “nafsi yake.”

Marejeo

  • +Mk 8:36; Lu 9:25
  • +Zb 49:8

Mathayo 16:27

Marejeo

  • +Zb 62:12; Met 24:12; Lu 9:26; Ro 2:6; 1Pe 1:17

Mathayo 16:28

Marejeo

  • +Mt 17:2; Mk 9:1; Lu 9:27

Jumla

Mt. 16:1Mt 12:38; Mk 8:11; Lu 11:16
Mt. 16:4Mk 8:12
Mt. 16:4Yon 1:17; Mt 12:39; Lu 11:29
Mt. 16:5Mk 8:13-21
Mt. 16:6Mk 8:15; Lu 12:1
Mt. 16:9Mt 14:17
Mt. 16:10Mt 15:34
Mt. 16:11Lu 12:1
Mt. 16:13Mk 8:27-29; Lu 9:18-20
Mt. 16:14Mt 14:1, 2
Mt. 16:14Yoh 1:25, 26
Mt. 16:16Mk 8:29; Lu 9:20; Yoh 1:40, 41; 4:25; 11:27
Mt. 16:16Zb 2:7; Mt 14:33; Mdo 9:20, 22; Ebr 1:2; 1Yo 4:15
Mt. 16:17Mt 11:27
Mt. 16:18Yoh 1:42
Mt. 16:18Ro 9:33; 1Ko 3:11; 10:4; Efe 2:20; 1Pe 2:6-8
Mt. 16:20Mk 8:29, 30; Lu 9:20, 21
Mt. 16:21Zb 16:10; Isa 53:12; Mt 17:22, 23; 20:18, 19; Mk 8:31; Lu 9:22; 24:46; 1Ko 15:3, 4
Mt. 16:22Mk 8:32
Mt. 16:23Mk 8:33
Mt. 16:24Mt 10:38; Mk 8:34; Lu 9:23; 14:27
Mt. 16:25Mk 8:35; Lu 9:24; 17:33; Yoh 12:25; Ufu 12:11
Mt. 16:26Mk 8:36; Lu 9:25
Mt. 16:26Zb 49:8
Mt. 16:27Zb 62:12; Met 24:12; Lu 9:26; Ro 2:6; 1Pe 1:17
Mt. 16:28Mt 17:2; Mk 9:1; Lu 9:27
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mathayo 16:1-28

Kulingana na Mathayo

16 Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu, na ili kumjaribu wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.+ 2 Akawajibu: “Inapofika jioni ninyi husema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri kwa maana anga ni jekundu,’ 3 na asubuhi mnasema: ‘Leo kutakuwa na baridi kali na mvua, kwa maana anga ni jekundu na lina mawingu mazito.’ Mnajua jinsi ya kufafanua hali ya anga, lakini hamwezi kufafanua ishara za nyakati. 4 Kizazi kiovu na chenye uzinzi* kinaendelea kutafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote+ isipokuwa ishara ya Yona.”+ Ndipo akawaacha, akaenda zake.

5 Sasa wanafunzi wakavuka kwenda ng’ambo ya bahari lakini wakasahau kuchukua mikate.+ 6 Yesu akawaambia: “Muwe macho na mjihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 7 Basi wakaanza kujadiliana, wakisema: “Hatukubeba mikate yoyote.” 8 Akijua hilo, Yesu akawauliza: “Ninyi wenye imani ndogo, kwa nini mnajadiliana kati yenu kuhusu kutokuwa na mikate? 9 Je, bado hamwelewi, au je, hamkumbuki ile mikate mitano kuhusiana na wale watu 5,000, na ni vikapu vingapi mlivyokusanya?+ 10 Au ile mikate saba kuhusiana na wale watu 4,000 na ni vikapu vingapi vikubwa mlivyokusanya?+ 11 Kwa nini hamwelewi kwamba sikuongea nanyi kuhusu mikate? Bali jihadharini na chachu* ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 12 Ndipo wakaelewa kwamba hakuwa akizungumza kuhusu chachu ya mikate, bali kujihadhari na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.

13 Alipofika katika eneo la Kaisaria Filipi, Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema Mwana wa binadamu ni nani?”+ 14 Wakajibu: “Baadhi yao husema Yohana Mbatizaji,+ wengine Eliya,+ na bado wengine Yeremia au mmoja wa manabii.” 15 Akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” 16 Simoni Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo,+ Mwana wa Mungu aliye hai.”+ 17 Yesu akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu mwili na damu havikukufunulia* hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.+ 18 Pia, ninakuambia: Wewe ni Petro,+ na juu ya mwamba+ huu nitajenga kutaniko langu, na malango ya Kaburi* hayatalishinda. 19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalofunga duniani tayari litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote utakalofungua duniani tayari litakuwa limefunguliwa mbinguni.” 20 Ndipo akawaagiza wanafunzi kwa kusisitiza wasimwambie yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.+

21 Tangu wakati huo, Yesu akaanza kuwafafanulia wanafunzi wake kwamba ni lazima aende Yerusalemu na kuteswa sana na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa, na siku ya tatu afufuliwe.+ 22 Ndipo Petro akampeleka kando na kuanza kumkemea, akisema: “Bwana jihurumie;* hutapatwa kamwe na mambo hayo.”+ 23 Lakini Yesu akamgeuzia mgongo, akamwambia Petro: “Nenda nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa sababu hufikirii mawazo ya Mungu, bali ya wanadamu.”+

24 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, aubebe mti wake wa mateso* na aendelee kunifuata.+ 25 Kwa maana yeyote anayetaka kuuokoa uhai wake* ataupoteza, lakini yeyote anayeupoteza uhai wake* kwa ajili yangu ataupata.+ 26 Kwa kweli mtu atapata faida gani akiupata ulimwengu wote lakini apoteze uhai wake?*+ Au mtu atatoa nini ili abadilishane na uhai wake?*+ 27 Kwa maana Mwana wa binadamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, kisha atamlipa kila mtu kulingana na mwenendo wake.+ 28 Kwa kweli ninawaambia kwamba kuna baadhi ya wale waliosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe kabla ya kumwona Mwana wa binadamu akija katika Ufalme wake.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki