Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 64
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Sala ya toba yaendelea (1-12)

        • Yehova “Mfinyanzi wetu” (8)

Isaya 64:3

Marejeo

  • +Kut 34:10
  • +Hab 3:6

Isaya 64:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kumngojea kwa subira.”

Marejeo

  • +Zb 130:6-8; Isa 25:9; Mik 7:7; 1Ko 2:9

Isaya 64:5

Marejeo

  • +Sef 2:3; Mdo 10:34, 35
  • +Isa 1:21; 63:10

Isaya 64:6

Marejeo

  • +Law 12:2; 15:20

Isaya 64:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “tuyeyuke.”

  • *

    Tnn., “kwa mkono wa.”

Marejeo

  • +Kum 31:17; Isa 57:17

Isaya 64:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Muumba wetu.”

Marejeo

  • +Isa 63:16
  • +Isa 29:16; 45:9; Yer 18:6

Isaya 64:9

Marejeo

  • +Zb 74:1; 79:5

Isaya 64:10

Marejeo

  • +Zb 79:1; Omb 1:4; 5:18; Mik 3:12

Isaya 64:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Hekalu letu la.”

  • *

    Au “uzuri.”

Marejeo

  • +2Nya 36:17, 19; Yer 52:12, 13

Isaya 64:12

Marejeo

  • +Zb 74:10, 11; Zek 1:12

Jumla

Isa. 64:3Kut 34:10
Isa. 64:3Hab 3:6
Isa. 64:4Zb 130:6-8; Isa 25:9; Mik 7:7; 1Ko 2:9
Isa. 64:5Sef 2:3; Mdo 10:34, 35
Isa. 64:5Isa 1:21; 63:10
Isa. 64:6Law 12:2; 15:20
Isa. 64:7Kum 31:17; Isa 57:17
Isa. 64:8Isa 63:16
Isa. 64:8Isa 29:16; 45:9; Yer 18:6
Isa. 64:9Zb 74:1; 79:5
Isa. 64:10Zb 79:1; Omb 1:4; 5:18; Mik 3:12
Isa. 64:112Nya 36:17, 19; Yer 52:12, 13
Isa. 64:12Zb 74:10, 11; Zek 1:12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 64:1-12

Isaya

64 Laiti ungezipasua mbingu ushuke chini,

Ili milima itetemeke kwa sababu yako,

 2 Kama moto unavyoteketeza vichaka,

Na moto huo unachemsha maji,

Basi jina lako litajulikana kwa maadui wako,

Na mataifa yatatetemeka mbele zako!

 3 Ulipofanya mambo yanayoogopesha ambayo hatungeweza kuyatazamia,+

Ulishuka, nayo milima ikatetemeka mbele zako.+

 4 Tangu zamani hakuna mtu aliyesikia wala kutega sikio,

Wala hakuna jicho lililomwona Mungu, isipokuwa wewe,

Yule anayetenda kwa ajili ya wale wanaoendelea kumtarajia.*+

 5 Umekutana na wale wanaoshangilia kutenda mambo yanayofaa,+

Wale wanaokukumbuka na kufuata njia zako.

Tazama! Ulikuwa na ghadhabu, huku sisi tukiendelea kutenda dhambi,+

Tulifanya hivyo kwa muda mrefu.

Je, sasa tuokolewe?

 6 Na sisi sote tumekuwa kama mtu asiye safi,

Na matendo yetu yote ya uadilifu ni kama kitambaa cha hedhi.+

Sisi sote tutanyauka kama jani,

Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.

 7 Hakuna yeyote anayeliitia jina lako,

Hakuna yeyote anayejichochea kukushika,

Kwa maana umeuficha uso wako kutoka kwetu,+

Nawe unatufanya tudhoofike* kwa sababu ya* kosa letu.

 8 Lakini sasa, Ee Yehova, wewe ni Baba yetu.+

Sisi ni udongo, nawe ni Mfinyanzi wetu;*+

Sisi sote ni kazi ya mkono wako.

 9 Usiwe na ghadhabu nyingi, Ee Yehova,+

Nawe usilikumbuke kosa letu milele.

Tafadhali, tutazame, kwa maana sisi sote ni watu wako.

10 Majiji yako matakatifu yamekuwa nyika.

Sayuni imekuwa nyika,

Yerusalemu limekuwa ukiwa.+

11 Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*

Ambamo mababu zetu walikusifu,

Imeteketezwa kwa moto,+

Na vitu vyote tulivyovithamini sana vimeharibiwa.

12 Baada ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova?

Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke kupita kiasi?+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki