Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 24
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Matendo—Yaliyomo

      • Mashtaka dhidi ya Paulo (1-9)

      • Paulo ajitetea mbele ya Feliksi (10-21)

      • Kesi ya Paulo yacheleweshwa kwa miaka miwili (22-27)

Matendo 24:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwanasheria.”

Marejeo

  • +Mdo 23:2
  • +Mdo 23:26

Matendo 24:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “tauni.”

Marejeo

  • +Mt 5:11; Mdo 16:20, 21; 17:6, 7
  • +Lu 23:1, 2
  • +Mt 2:23; Mdo 28:22

Matendo 24:6

Marejeo

  • +Mdo 21:27, 28

Matendo 24:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A3.

Matendo 24:10

Marejeo

  • +Flp 1:7

Matendo 24:11

Marejeo

  • +Mdo 21:17, 26

Matendo 24:14

Marejeo

  • +Kut 3:15; Mdo 3:13; 2Ti 1:3
  • +Mdo 28:23; Ro 3:21

Matendo 24:15

Marejeo

  • +Isa 26:19; Mt 22:31, 32; Lu 14:13, 14; Yoh 5:28, 29; 11:25; Ebr 11:35; Ufu 20:12
  • +Lu 23:43

Matendo 24:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “dhamiri isiyo na lawama.”

Marejeo

  • +Mdo 23:1; 1Ko 4:4; Ebr 13:18

Matendo 24:17

Marejeo

  • +2Ko 8:4

Matendo 24:18

Marejeo

  • +Mdo 21:24, 26

Matendo 24:19

Marejeo

  • +Mdo 25:16

Matendo 24:21

Marejeo

  • +Mdo 23:6

Matendo 24:22

Marejeo

  • +Mdo 9:1, 2; 19:9

Matendo 24:24

Marejeo

  • +Mt 10:18

Matendo 24:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kujidhibiti; kujiweza.”

Marejeo

  • +Mdo 17:30, 31; 2Ko 5:10

Matendo 24:27

Marejeo

  • +Mdo 25:9

Jumla

Mdo. 24:1Mdo 23:2
Mdo. 24:1Mdo 23:26
Mdo. 24:5Mt 5:11; Mdo 16:20, 21; 17:6, 7
Mdo. 24:5Lu 23:1, 2
Mdo. 24:5Mt 2:23; Mdo 28:22
Mdo. 24:6Mdo 21:27, 28
Mdo. 24:10Flp 1:7
Mdo. 24:11Mdo 21:17, 26
Mdo. 24:14Kut 3:15; Mdo 3:13; 2Ti 1:3
Mdo. 24:14Mdo 28:23; Ro 3:21
Mdo. 24:15Isa 26:19; Mt 22:31, 32; Lu 14:13, 14; Yoh 5:28, 29; 11:25; Ebr 11:35; Ufu 20:12
Mdo. 24:15Lu 23:43
Mdo. 24:16Mdo 23:1; 1Ko 4:4; Ebr 13:18
Mdo. 24:172Ko 8:4
Mdo. 24:18Mdo 21:24, 26
Mdo. 24:19Mdo 25:16
Mdo. 24:21Mdo 23:6
Mdo. 24:22Mdo 9:1, 2; 19:9
Mdo. 24:24Mt 10:18
Mdo. 24:25Mdo 17:30, 31; 2Ko 5:10
Mdo. 24:27Mdo 25:9
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Matendo 24:1-27

Matendo ya Mitume

24 Siku tano baadaye kuhani mkuu Anania+ akashuka pamoja na baadhi ya wazee na msemaji wa hadharani* aliyeitwa Tertulo, nao wakawasilisha kesi yao dhidi ya Paulo mbele ya gavana.+ 2 Alipoitwa, Tertulo akaanza kumshtaki, akisema:

“Kwa kuwa tunafurahia amani nyingi kupitia kwako, na kwa busara yako mabadiliko yanatokea katika taifa hili, 3 nyakati zote na kila mahali tunatambua jambo hilo kwa shukrani nyingi sana, ewe Mtukufu Feliksi. 4 Lakini ili nisitumie muda wako mwingi, ninakuomba kwa fadhili zako utusikilize kwa ufupi. 5 Kwa maana tumemwona mtu huyu kuwa msumbufu,*+ akichochea uasi+ miongoni mwa Wayahudi wote katika dunia yote inayokaliwa, naye ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazareti.+ 6 Pia alijaribu kulichafua hekalu, basi tukamkamata.+ 7* —— 8 Wewe mwenyewe utakapomhoji, utagundua mambo haya yote ambayo tunamshtaki.”

9 Ndipo Wayahudi pia wakajiunga katika shambulio hilo, wakisisitiza kwamba mambo hayo ni ya kweli. 10 Gavana alipomtolea Paulo ishara ili azungumze, akajibu:

“Ninajua vema kwamba umekuwa mwamuzi wa taifa hili kwa miaka mingi, nami nafurahi kujitetea mbele yako.+ 11 Unaweza kujihakikishia kwamba hazijapita zaidi ya siku 12 tangu nilipopanda kwenda kuabudu huko Yerusalemu;+ 12 nao hawakunipata hekaluni nikibishana na mtu yeyote wala kuchochea kikundi chenye ghasia, katika masinagogi au kotekote jijini. 13 Wala hawawezi kukuthibitishia mambo wanayonishtaki sasa hivi. 14 Lakini ninakiri jambo hili kwako, kwamba kulingana na njia wanayoiita ‘madhehebu,’ hivyo ndivyo ninavyomtolea utumishi mtakatifu Mungu wa mababu zangu,+ kwa kuwa ninaamini mambo yote yaliyo katika Sheria na yaliyoandikwa katika Manabii.+ 15 Nami nina tumaini kwa Mungu, tumaini ambalo watu hawa pia wanatazamia, kwamba kutakuwa na ufufuo+ wa waadilifu na wasio waadilifu pia.+ 16 Kwa sababu hiyo sikuzote ninajitahidi kudumisha dhamiri safi* mbele za Mungu na wanadamu.+ 17 Sasa baada ya miaka kadhaa, nilirudi ili kuleta zawadi za rehema+ kwa taifa langu na kutoa matoleo. 18 Nilipokuwa nikishughulikia mambo hayo, walinikuta hekaluni nikiwa nimetakaswa kisherehe,+ lakini sikuwa na umati wala sikuwa ninasababisha fujo. Lakini kulikuwa na Wayahudi fulani kutoka mkoa wa Asia 19 ambao wanapaswa kuwa hapa mbele yako ili wanishtaki ikiwa kwa kweli wana jambo lolote dhidi yangu.+ 20 Au uwaambie watu walio hapa waseme wenyewe kosa walilopata nilipokuwa nimesimama mbele ya Sanhedrini, 21 isipokuwa jambo hili moja nililosema kwa sauti kubwa nilipokuwa nimesimama kati yao: ‘Mimi ninahukumiwa leo mbele yenu kwa sababu ya ufufuo wa wafu!’”+

22 Hata hivyo, Feliksi, akiwa anajua vizuri ukweli kuhusu Njia hii,+ akaahirisha kesi yao kwa kusema: “Lisia kamanda wa jeshi atakapokuja, nitaamua mambo haya yanayowahusu.” 23 Naye akamwagiza ofisa wa jeshi kwamba mtu huyo awekwe chini ya kizuizi lakini apewe uhuru fulani, na watu wake waruhusiwe kumhudumia.

24 Siku kadhaa baadaye Feliksi akaja na Drusila mke wake, aliyekuwa Myahudi, akawatuma watu wamwite Paulo naye akamsikiliza akizungumza kuhusu imani katika Kristo Yesu.+ 25 Lakini Paulo alipokuwa akiongea kuhusu uadilifu na kujizuia* na hukumu itakayokuja,+ Feliksi akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kwenda, lakini nitakapopata nafasi nitakuita tena.” 26 Wakati huohuo alitumaini kwamba Paulo angempa pesa. Kwa hiyo, akamwita mara nyingi na kuzungumza naye. 27 Lakini miaka miwili ilipokwisha, Porkio Festo alichukua nafasi ya Feliksi; na kwa sababu Feliksi alitamani kukubaliwa na Wayahudi,+ akamwacha Paulo akiwa amefungwa.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki