Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Waamuzi—Yaliyomo

      • Wamidiani wawakandamiza Waisraeli (1-10)

      • Malaika amhakikishia Mwamuzi Gideoni atapata msaada (11-24)

      • Gideoni abomoa madhabahu ya Baali (25-32)

      • Roho ya Mungu yamtia nguvu Gideoni (33-35)

      • Jaribio la manyoya (36-40)

Waamuzi 6:1

Marejeo

  • +Amu 2:19
  • +Kum 28:15, 48; Amu 2:14; Ne 9:28

Waamuzi 6:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “maghala yaliyo chini ya ardhi.”

Marejeo

  • +Hes 33:55
  • +1Sa 13:5, 6

Waamuzi 6:3

Marejeo

  • +Amu 3:13
  • +Amu 8:10

Waamuzi 6:4

Marejeo

  • +Kum 28:15, 33; 28:31, 48

Waamuzi 6:5

Marejeo

  • +Amu 8:10
  • +Amu 7:12

Waamuzi 6:6

Marejeo

  • +Kum 4:30

Waamuzi 6:7

Marejeo

  • +Amu 2:18; Zb 107:19

Waamuzi 6:8

Marejeo

  • +Kut 20:2; Law 26:13; Amu 2:1

Waamuzi 6:9

Marejeo

  • +Yos 10:42; Ne 9:24

Waamuzi 6:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “hamkuisikiliza sauti yangu.”

Marejeo

  • +Kum 6:4
  • +Yos 24:15
  • +Kum 28:15; Amu 2:2; Yer 3:13

Waamuzi 6:11

Marejeo

  • +Amu 2:1
  • +Yos 17:2; Amu 6:24; 8:32
  • +Mwa 49:22, 24; Ebr 11:32

Waamuzi 6:12

Marejeo

  • +Amu 2:18

Waamuzi 6:13

Marejeo

  • +Amu 6:2
  • +Kum 4:9; Zb 44:1
  • +Kut 13:14
  • +Kum 31:17; 2Nya 15:2

Waamuzi 6:14

Marejeo

  • +Amu 8:22; Ebr 11:32

Waamuzi 6:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Elfu yangu ndiyo ndogo.”

Waamuzi 6:16

Marejeo

  • +Kum 20:3, 4; Amu 2:18

Waamuzi 6:18

Marejeo

  • +Mwa 18:3, 5; Amu 13:15

Waamuzi 6:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Efa ya unga ilikuwa karibu kilogramu 13. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Mwa 18:6, 7; 19:1, 3

Waamuzi 6:21

Marejeo

  • +Law 9:24; Amu 13:19, 20; 1Fa 18:38; 1Nya 21:26; 2Nya 7:1

Waamuzi 6:22

Marejeo

  • +Amu 13:8, 9; Ebr 13:2
  • +Mwa 16:7, 13; 32:24, 30; Amu 13:21, 22; Lu 1:11, 12

Waamuzi 6:23

Marejeo

  • +Da 10:19

Waamuzi 6:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Yehova Ni Amani.”

Marejeo

  • +Mwa 22:14; Kut 17:15

Waamuzi 6:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Kut 23:24; Kum 12:3

Waamuzi 6:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Waamuzi 6:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Waamuzi 6:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Waamuzi 6:31

Marejeo

  • +Amu 6:11
  • +Kum 13:5; 17:2-5
  • +1Fa 18:26, 27; Zb 115:5; Yer 10:5

Waamuzi 6:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Acheni Baali Ajitetee Kisheria (Apambane).”

Waamuzi 6:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wakavuka mto.”

  • *

    Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”

Marejeo

  • +Hes 25:17, 18; Amu 6:2
  • +Kut 17:16; Hes 24:20; Kum 25:19
  • +Amu 6:3; 7:12

Waamuzi 6:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ikamfunika.”

  • *

    Au “tarumbeta.”

Marejeo

  • +Amu 3:9, 10; 11:29; 13:24, 25; 14:6; 15:14; Zek 4:6
  • +Amu 3:26, 27
  • +Yos 17:2

Waamuzi 6:36

Marejeo

  • +Amu 6:14

Jumla

Amu. 6:1Amu 2:19
Amu. 6:1Kum 28:15, 48; Amu 2:14; Ne 9:28
Amu. 6:2Hes 33:55
Amu. 6:21Sa 13:5, 6
Amu. 6:3Amu 3:13
Amu. 6:3Amu 8:10
Amu. 6:4Kum 28:15, 33; 28:31, 48
Amu. 6:5Amu 8:10
Amu. 6:5Amu 7:12
Amu. 6:6Kum 4:30
Amu. 6:7Amu 2:18; Zb 107:19
Amu. 6:8Kut 20:2; Law 26:13; Amu 2:1
Amu. 6:9Yos 10:42; Ne 9:24
Amu. 6:10Kum 6:4
Amu. 6:10Yos 24:15
Amu. 6:10Kum 28:15; Amu 2:2; Yer 3:13
Amu. 6:11Amu 2:1
Amu. 6:11Yos 17:2; Amu 6:24; 8:32
Amu. 6:11Mwa 49:22, 24; Ebr 11:32
Amu. 6:12Amu 2:18
Amu. 6:13Amu 6:2
Amu. 6:13Kum 4:9; Zb 44:1
Amu. 6:13Kut 13:14
Amu. 6:13Kum 31:17; 2Nya 15:2
Amu. 6:14Amu 8:22; Ebr 11:32
Amu. 6:16Kum 20:3, 4; Amu 2:18
Amu. 6:18Mwa 18:3, 5; Amu 13:15
Amu. 6:19Mwa 18:6, 7; 19:1, 3
Amu. 6:21Law 9:24; Amu 13:19, 20; 1Fa 18:38; 1Nya 21:26; 2Nya 7:1
Amu. 6:22Amu 13:8, 9; Ebr 13:2
Amu. 6:22Mwa 16:7, 13; 32:24, 30; Amu 13:21, 22; Lu 1:11, 12
Amu. 6:23Da 10:19
Amu. 6:24Mwa 22:14; Kut 17:15
Amu. 6:25Kut 23:24; Kum 12:3
Amu. 6:31Amu 6:11
Amu. 6:31Kum 13:5; 17:2-5
Amu. 6:311Fa 18:26, 27; Zb 115:5; Yer 10:5
Amu. 6:33Hes 25:17, 18; Amu 6:2
Amu. 6:33Kut 17:16; Hes 24:20; Kum 25:19
Amu. 6:33Amu 6:3; 7:12
Amu. 6:34Amu 3:9, 10; 11:29; 13:24, 25; 14:6; 15:14; Zek 4:6
Amu. 6:34Amu 3:26, 27
Amu. 6:34Yos 17:2
Amu. 6:36Amu 6:14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Waamuzi 6:1-40

Waamuzi

6 Lakini Waisraeli wakatenda tena mambo maovu machoni pa Yehova,+ basi Yehova akawatia mikononi mwa Wamidiani kwa miaka saba.+ 2 Na Wamidiani wakawakandamiza Waisraeli.+ Kwa sababu ya Wamidiani, Waisraeli wakachimba mashimo ya kujificha* katika milima, mapango, na mahali pagumu kufikiwa.+ 3 Waisraeli walipopanda mbegu, Wamidiani, Waamaleki,+ na watu wa Mashariki+ waliwashambulia. 4 Nao walikuwa wakipiga kambi ili kuwashambulia na kuharibu mazao yote nchini hadi Gaza, na hawakuwaachia Waisraeli chakula chochote, wala kondoo, ng’ombe dume, au punda.+ 5 Walikuja na mifugo yao na mahema mengi sana kama nzige,+ na wao pamoja na ngamia wao hawangeweza kuhesabiwa,+ walikuja ili kuiharibu nchi. 6 Basi Wamidiani wakawafanya Waisraeli kuwa maskini sana; na Waisraeli wakamlilia Yehova awasaidie.+

7 Waisraeli walipomlilia Yehova awasaidie kwa sababu ya Wamidiani,+ 8 Yehova aliwaletea Waisraeli nabii aliyewaambia hivi: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Niliwatoa Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+ 9 Nikawaokoa kutoka mikononi mwa Wamisri na mikononi mwa wote waliowakandamiza, nikawafukuza mbele yenu na kuwapa ninyi nchi yao.+ 10 Kisha nikawaambia, “Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ Msiogope miungu ya Waamori ambao mnakaa katika nchi yao.”+ Lakini hamkunitii.’”*+

11 Baadaye malaika wa Yehova akaja+ na kuketi chini ya mti mkubwa wa Yoashi Mwabiezeri uliokuwa Ofra.+ Gideoni mwanawe+ alikuwa akipura ngano katika shinikizo la divai ili Wamidiani wasiione. 12 Ndipo malaika wa Yehova akamtokea, akamwambia hivi: “Yehova yuko pamoja nawe,+ ewe shujaa hodari.” 13 Gideoni akamwambia, “Niwie radhi, bwana wangu, lakini ikiwa Yehova yuko pamoja nasi, kwa nini mambo haya yote yametupata?+ Yako wapi matendo yake ya ajabu ambayo baba zetu walitusimulia,+ wakisema, ‘Yehova ndiye aliyetutoa Misri?’+ Sasa Yehova ametuacha,+ naye ametutia mikononi mwa Wamidiani.” 14 Ndipo Yehova akamgeukia na kumwambia, “Nenda kwa nguvu ulizo nazo, nawe utawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamidiani.+ Je, si mimi ninayekutuma?” 15 Gideoni akamjibu, “Niwie radhi, Yehova. Ninawezaje kuwaokoa Waisraeli? Ukoo wangu ndio mdogo* zaidi katika kabila la Manase, nami ni mdogo kabisa katika nyumba ya baba yangu.” 16 Lakini Yehova akamwambia, “Kwa sababu nitakuwa pamoja nawe,+ utawashinda Wamidiani kana kwamba ni mtu mmoja.”

17 Ndipo Gideoni akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, nionyeshe ishara kwamba ni wewe unayeongea nami. 18 Tafadhali usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea zawadi yangu na kuiweka mbele yako.”+ Basi akasema, “Sitaondoka mpaka utakaporudi.” 19 Kwa hiyo Gideoni akaingia nyumbani na kutayarisha mwanambuzi na kuoka mikate isiyo na chachu kwa kutumia efa* ya unga.+ Akaweka nyama katika kikapu na kutia mchuzi katika chungu cha kupikia; kisha akampelekea chini ya ule mti mkubwa.

20 Sasa yule malaika wa Mungu wa kweli akamwambia, “Chukua nyama na mikate hiyo isiyo na chachu, uviweke juu ya lile jiwe kubwa, na umimine mchuzi juu yake.” Akafanya hivyo. 21 Ndipo malaika wa Yehova akanyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kwa ncha yake akaigusa ile nyama na ile mikate isiyo na chachu, na moto ukatoka kwenye lile jiwe na kuiteketeza ile nyama na ile mikate isiyo na chachu.+ Kisha malaika wa Yehova akatoweka. 22 Ndipo Gideoni akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yehova.+

Mara moja Gideoni akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kwa sababu nimemwona malaika wa Yehova uso kwa uso!”+ 23 Lakini Yehova akamwambia, “Uwe na amani. Usiogope;+ hutakufa.” 24 Basi Gideoni akamjengea Yehova madhabahu hapo, ambayo mpaka leo hii inaitwa Yehova-shalomu.*+ Bado iko huko Ofra ya Waabiezeri.

25 Usiku huo Yehova akamwambia, “Mchukue ng’ombe dume mchanga wa baba yako, ng’ombe dume mchanga wa pili mwenye miaka saba, nawe ubomoe madhabahu ya Baali ambayo ni ya baba yako, na ukate mti mtakatifu* ulio kando yake.+ 26 Baada ya kumjengea Yehova Mungu wako madhabahu juu ya ngome hii kwa mawe yaliyopangwa vizuri, mchukue yule ng’ombe dume mchanga wa pili unitolee dhabihu ya kuteketezwa juu ya kuni za ule mti mtakatifu* ambao ulikata.” 27 Basi Gideoni akawachukua wanaume kumi kati ya watumishi wake na kufanya kama Yehova alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa sana watu wa nyumba ya baba yake na wakaaji wa jiji, hakufanya mambo hayo mchana, aliyafanya usiku.

28 Wakaaji wa jiji walipoamka asubuhi na mapema, waliona kwamba madhabahu ya Baali ilikuwa imebomolewa na ule mti mtakatifu* uliokuwa kando yake ulikuwa umekatwa, na yule ng’ombe dume mchanga wa pili alikuwa ameteketezwa juu ya madhabahu iliyokuwa imejengwa. 29 Wakaulizana, “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Baada ya kufanya uchunguzi, wakasema, “Gideoni mwana wa Yoashi ndiye aliyefanya jambo hili.” 30 Kwa hiyo wakaaji wa jiji wakamwambia hivi Yoashi: “Mtoe nje mwana wako, anapaswa kufa kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukata mti mtakatifu* uliokuwa kando yake.” 31 Ndipo Yoashi+ akawaambia watu wote waliomkabili, “Je, ni lazima mumtetee Baali? Je, ni lazima mumwokoe? Yeyote anayemtetea anapaswa kuuawa asubuhi hii.+ Ikiwa yeye ni mungu, acheni ajitetee mwenyewe,+ kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.” 32 Siku hiyo akamwita Gideoni jina Yerubaali,* akisema, “Acheni Baali ajitetee mwenyewe, kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.”

33 Wamidiani wote+ na Waamaleki+ na watu wa Mashariki wakaungana;+ wakavuka* na kupiga kambi katika Bonde la* Yezreeli. 34 Kisha roho ya Yehova ikamjia* Gideoni+ naye akapiga pembe,*+ na Waabiezeri+ wakakusanyika na kumfuata. 35 Akatuma wajumbe katika nchi yote ya kabila la Manase, wakakusanyika pia na kumfuata. Akatuma pia wajumbe kotekote katika nchi ya Asheri, Zabuloni, na Naftali, nao wakaja kukutana naye.

36 Kisha Gideoni akamwambia hivi Mungu wa kweli: “Ikiwa utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi,+ 37 ninaweka manyoya ya kondoo kwenye uwanja wa kupuria. Ikiwa kutakuwa na umande juu ya manyoya hayo peke yake lakini ardhi yote inayozunguka manyoya hayo iwe kavu, ndipo nitakapojua kwamba utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi.” 38 Na ikawa hivyo. Alipoamka mapema siku iliyofuata na kukamua manyoya hayo, maji ya umande yalijaa kwenye bakuli kubwa. 39 Hata hivyo, Gideoni akamwambia hivi Mungu wa kweli: “Tafadhali usinikasirikie, nakuomba jambo moja zaidi. Tafadhali niruhusu nifanye jaribio lingine moja tu kwa manyoya haya. Tafadhali, acha manyoya peke yake yawe makavu, na ardhi yote iwe na umande.” 40 Basi Mungu akafanya hivyo usiku huo; manyoya peke yake yakawa makavu, na ardhi yote ikawa na umande.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki