Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 2
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Mungu apumzika siku ya saba (1-3)

      • Yehova Mungu, Muumbaji wa mbingu na dunia (4)

      • Mwanamume na mwanamke katika bustani ya Edeni (5-25)

        • Mtu aumbwa kutokana na mavumbi (7)

        • Mti uliokatazwa wa ujuzi (15-17)

        • Kuumbwa kwa mwanamke (18-25)

Mwanzo 2:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “na jeshi lake lote likakamilika.”

Marejeo

  • +Ne 9:6; Zb 146:6

Mwanzo 2:2

Marejeo

  • +Kut 31:17; Ebr 4:4

Mwanzo 2:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Hili ndilo andiko la kwanza kutaja jina la pekee la Mungu, יהוה (YHWH). Angalia Nyongeza A4.

Marejeo

  • +Isa 45:18

Mwanzo 2:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi hai.” Kiebrania, neʹphesh, ambalo kihalisi linamaanisha “kiumbe anayepumua.” Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Mwa 3:19; Zb 103:14; Mhu 3:20
  • +Mwa 7:22; Isa 42:5; Mdo 17:25
  • +1Ko 15:45, 47

Mwanzo 2:8

Marejeo

  • +Mwa 2:15; 3:23
  • +Mwa 1:26

Mwanzo 2:9

Marejeo

  • +Mwa 3:22, 24; Ufu 2:7
  • +Mwa 2:17

Mwanzo 2:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “na kuwa vichwa vinne.”

Mwanzo 2:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Tigri.”

Marejeo

  • +Da 10:4
  • +Mwa 10:8, 11
  • +Mwa 15:18; Kum 11:24

Mwanzo 2:15

Marejeo

  • +Mwa 1:28; 2:8; Zb 115:16

Mwanzo 2:16

Marejeo

  • +Mwa 2:8, 9; 3:2

Mwanzo 2:17

Marejeo

  • +Mwa 3:19; Zb 146:4; Mhu 9:5, 10; Eze 18:4; Ro 5:12; 1Ko 15:22

Mwanzo 2:18

Marejeo

  • +1Ko 11:8, 9; 1Ti 2:13

Mwanzo 2:19

Marejeo

  • +Mwa 1:26

Mwanzo 2:22

Marejeo

  • +Mk 10:9; 1Ti 2:13

Mwanzo 2:23

Marejeo

  • +1Ko 11:8

Mwanzo 2:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ataendelea kuwa.”

Marejeo

  • +Mal 2:16; Mt 19:5; Mk 10:7, 8; Ro 7:2; 1Ko 6:16; Efe 5:31; Ebr 13:4

Mwanzo 2:25

Marejeo

  • +Mwa 3:7

Jumla

Mwa. 2:1Ne 9:6; Zb 146:6
Mwa. 2:2Kut 31:17; Ebr 4:4
Mwa. 2:4Isa 45:18
Mwa. 2:7Mwa 3:19; Zb 103:14; Mhu 3:20
Mwa. 2:7Mwa 7:22; Isa 42:5; Mdo 17:25
Mwa. 2:71Ko 15:45, 47
Mwa. 2:8Mwa 2:15; 3:23
Mwa. 2:8Mwa 1:26
Mwa. 2:9Mwa 3:22, 24; Ufu 2:7
Mwa. 2:9Mwa 2:17
Mwa. 2:14Da 10:4
Mwa. 2:14Mwa 10:8, 11
Mwa. 2:14Mwa 15:18; Kum 11:24
Mwa. 2:15Mwa 1:28; 2:8; Zb 115:16
Mwa. 2:16Mwa 2:8, 9; 3:2
Mwa. 2:17Mwa 3:19; Zb 146:4; Mhu 9:5, 10; Eze 18:4; Ro 5:12; 1Ko 15:22
Mwa. 2:181Ko 11:8, 9; 1Ti 2:13
Mwa. 2:19Mwa 1:26
Mwa. 2:22Mk 10:9; 1Ti 2:13
Mwa. 2:231Ko 11:8
Mwa. 2:24Mal 2:16; Mt 19:5; Mk 10:7, 8; Ro 7:2; 1Ko 6:16; Efe 5:31; Ebr 13:4
Mwa. 2:25Mwa 3:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 2:1-25

Mwanzo

2 Basi mbingu na dunia na kila kitu kilichomo vikakamilika.*+ 2 Na kufikia siku ya saba, Mungu alikuwa amemaliza kazi aliyokuwa akifanya, naye akaanza kupumzika siku ya saba kutoka katika kazi yake yote aliyokuwa amefanya.+ 3 Na Mungu akaibariki siku ya saba na kuitangaza kuwa takatifu, kwa kuwa katika siku hiyo Mungu amekuwa akipumzika kutokana na kazi yake yote ya kuumba, vyote alivyokusudia kuumba.

4 Hii ndiyo historia ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa, siku ambayo Yehova* Mungu aliumba dunia na mbingu.+

5 Dunia bado haikuwa na kichaka chochote na hakuna mmea wowote uliokuwa umeanza kuchipuka, kwa sababu Yehova Mungu hakuwa amefanya mvua inyeshe duniani na hapakuwa na mtu wa kuilima ardhi. 6 Lakini ukungu ulikuwa ukipanda kutoka duniani, nao uliinywesha ardhi yote.

7 Kisha Yehova Mungu akamuumba mtu kutokana na mavumbi+ ya ardhi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai,+ na mtu huyo akawa mtu aliye hai.*+ 8 Zaidi ya hilo, Yehova Mungu akapanda bustani kule Edeni,+ kuelekea mashariki; na humo akamweka huyo mtu aliyemuumba.+ 9 Kwa hiyo Yehova Mungu akachipusha ardhini kila mti wenye kupendeza macho na unaofaa kwa chakula na pia mti wa uzima+ katikati ya bustani na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.+

10 Sasa kulikuwa na mto uliotiririka kutoka Edeni ili kuinywesha bustani, na kutoka huko uligawanyika na kuwa mito minne.* 11 Jina la mto wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu. 12 Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri. Pia kuna utomvu wa mbedola na madini ya shohamu. 13 Jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. 14 Jina la mto wa tatu ni Hidekeli;*+ ndio unaoelekea upande wa mashariki wa Ashuru.+ Na mto wa nne ni Efrati.+

15 Yehova Mungu akamchukua huyo mtu na kumweka katika bustani ya Edeni ili ailime na kuitunza.+ 16 Pia, Yehova Mungu akampa huyo mtu amri hii: “Unaweza kula matunda ya kila mti katika bustani mpaka ushibe.+ 17 Lakini kuhusu mti wa ujuzi wa mema na mabaya, usile matunda yake, kwa maana siku utakapokula matunda yake hakika utakufa.”+

18 Kisha Yehova Mungu akasema: “Si vema mwanamume huyu aendelee kuwa peke yake. Nitamuumbia msaidizi, awe kikamilisho chake.”+ 19 Sasa Yehova Mungu aliumba kutoka mavumbini kila mnyama wa mwituni na kila kiumbe anayeruka angani, naye akaanza kuwaleta kwa mtu huyo ili aamue jina atakalompa kila kiumbe; na jina lolote ambalo mtu huyo alimpa kila kiumbe aliye hai, likawa jina lake.+ 20 Basi mtu huyo akawapa majina wanyama wote wa kufugwa na viumbe wote wanaoruka angani na kila mnyama wa mwituni, lakini mwanamume huyo hakuwa na msaidizi ambaye angekuwa kikamilisho chake. 21 Kwa hiyo Yehova Mungu akamletea mwanamume huyo usingizi mzito, na alipokuwa akilala, akachukua ubavu wake mmoja na kufunika nyama mahali hapo. 22 Na Yehova Mungu akaufanya ubavu aliochukua kutoka kwa mwanamume uwe mwanamke, naye akamleta kwa mwanamume huyo.+

23 Ndipo mwanamume huyo akasema:

“Hatimaye huyu ni mfupa wa mifupa yangu

Na nyama ya nyama yangu.

Huyu ataitwa Mwanamke,

Kwa sababu alitolewa+ katika mwanamume.”

24 Ndiyo sababu mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana* na mke wake, nao watakuwa mwili mmoja.+ 25 Na wote wawili wakaendelea kuwa uchi,+ huyo mwanamume na mke wake; lakini hawakuona aibu.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki