Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Hesabu—Yaliyomo

      • Tarumbeta za fedha (1-10)

      • Kuondoka Sinai (11-13)

      • Utaratibu wa kuondoka (14-28)

      • Hobabu aombwa awaongoze Waisraeli (29-34)

      • Sala aliyotoa Musa walipokuwa wakianza safari (35, 36)

Hesabu 10:2

Marejeo

  • +Law 23:24

Hesabu 10:3

Marejeo

  • +Hes 1:18; Kum 29:10, 11

Hesabu 10:4

Marejeo

  • +Kut 18:21; Hes 1:16; 7:2; Kum 1:15; 5:23

Hesabu 10:5

Marejeo

  • +Hes 2:3

Hesabu 10:6

Marejeo

  • +Hes 2:10

Hesabu 10:7

Marejeo

  • +Hes 10:3

Hesabu 10:8

Marejeo

  • +Hes 31:6; 1Nya 15:24; 16:6; 2Nya 29:26; Ne 12:35, 41

Hesabu 10:9

Marejeo

  • +2Nya 13:12

Hesabu 10:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “juu ya.”

Marejeo

  • +1Nya 15:28; 2Nya 5:12; 7:6; Ezr 3:10
  • +Law 23:24; Hes 29:1
  • +Hes 28:11
  • +Law 3:1
  • +Kut 6:7; Law 11:45

Hesabu 10:11

Marejeo

  • +Hes 1:1
  • +Hes 9:17; Zb 78:14

Hesabu 10:12

Marejeo

  • +Kut 40:36; Hes 2:9, 16, 17, 24, 31
  • +Hes 12:16; 13:26; Kum 1:1, 2

Hesabu 10:13

Marejeo

  • +Hes 2:34; 9:23

Hesabu 10:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “majeshi yake.”

Marejeo

  • +Hes 1:4, 7; 2:3

Hesabu 10:15

Marejeo

  • +Hes 1:4, 8; 2:5

Hesabu 10:16

Marejeo

  • +Hes 2:7

Hesabu 10:17

Marejeo

  • +Hes 1:51
  • +Hes 3:25, 26
  • +Hes 3:36, 37

Hesabu 10:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “majeshi yake.”

Marejeo

  • +Hes 1:4, 5; 2:10

Hesabu 10:19

Marejeo

  • +Hes 1:5, 6; 2:12

Hesabu 10:20

Marejeo

  • +Hes 1:4, 14; 2:14

Hesabu 10:21

Marejeo

  • +Hes 3:30, 31; 4:15; 7:9

Hesabu 10:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “majeshi yake.”

Marejeo

  • +Hes 1:4, 10; 2:18, 24

Hesabu 10:23

Marejeo

  • +Hes 1:4, 10; 2:20

Hesabu 10:24

Marejeo

  • +Hes 1:4, 11; 2:22

Hesabu 10:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “majeshi yake.”

Marejeo

  • +Hes 1:4, 12; 2:25, 31

Hesabu 10:26

Marejeo

  • +Hes 1:4, 13; 2:27

Hesabu 10:27

Marejeo

  • +Hes 1:4, 15; 2:29

Hesabu 10:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “majeshi yao yalifuata.”

Marejeo

  • +Hes 2:34

Hesabu 10:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, Yethro.

Marejeo

  • +Kut 2:16, 18; 3:1; 18:1, 5
  • +Mwa 12:7; 13:14, 15; 15:18
  • +Amu 1:16; 4:11; 1Sa 15:6
  • +Kut 3:8; 6:7

Hesabu 10:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuwa macho yetu.”

Hesabu 10:32

Marejeo

  • +Amu 1:16; 4:11

Hesabu 10:33

Marejeo

  • +Kut 3:1; 19:3; 24:16; Kum 5:2
  • +Kut 25:10, 17
  • +Kum 1:32, 33; Yos 3:3, 4

Hesabu 10:34

Marejeo

  • +Kut 13:21; Ne 9:12; Zb 78:14

Hesabu 10:35

Marejeo

  • +Zb 132:8

Hesabu 10:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “makumi ya maelfu kwa maelfu.”

Marejeo

  • +Kum 1:10

Jumla

Hes. 10:2Law 23:24
Hes. 10:3Hes 1:18; Kum 29:10, 11
Hes. 10:4Kut 18:21; Hes 1:16; 7:2; Kum 1:15; 5:23
Hes. 10:5Hes 2:3
Hes. 10:6Hes 2:10
Hes. 10:7Hes 10:3
Hes. 10:8Hes 31:6; 1Nya 15:24; 16:6; 2Nya 29:26; Ne 12:35, 41
Hes. 10:92Nya 13:12
Hes. 10:101Nya 15:28; 2Nya 5:12; 7:6; Ezr 3:10
Hes. 10:10Law 23:24; Hes 29:1
Hes. 10:10Hes 28:11
Hes. 10:10Law 3:1
Hes. 10:10Kut 6:7; Law 11:45
Hes. 10:11Hes 1:1
Hes. 10:11Hes 9:17; Zb 78:14
Hes. 10:12Kut 40:36; Hes 2:9, 16, 17, 24, 31
Hes. 10:12Hes 12:16; 13:26; Kum 1:1, 2
Hes. 10:13Hes 2:34; 9:23
Hes. 10:14Hes 1:4, 7; 2:3
Hes. 10:15Hes 1:4, 8; 2:5
Hes. 10:16Hes 2:7
Hes. 10:17Hes 1:51
Hes. 10:17Hes 3:25, 26
Hes. 10:17Hes 3:36, 37
Hes. 10:18Hes 1:4, 5; 2:10
Hes. 10:19Hes 1:5, 6; 2:12
Hes. 10:20Hes 1:4, 14; 2:14
Hes. 10:21Hes 3:30, 31; 4:15; 7:9
Hes. 10:22Hes 1:4, 10; 2:18, 24
Hes. 10:23Hes 1:4, 10; 2:20
Hes. 10:24Hes 1:4, 11; 2:22
Hes. 10:25Hes 1:4, 12; 2:25, 31
Hes. 10:26Hes 1:4, 13; 2:27
Hes. 10:27Hes 1:4, 15; 2:29
Hes. 10:28Hes 2:34
Hes. 10:29Kut 2:16, 18; 3:1; 18:1, 5
Hes. 10:29Mwa 12:7; 13:14, 15; 15:18
Hes. 10:29Amu 1:16; 4:11; 1Sa 15:6
Hes. 10:29Kut 3:8; 6:7
Hes. 10:32Amu 1:16; 4:11
Hes. 10:33Kut 3:1; 19:3; 24:16; Kum 5:2
Hes. 10:33Kut 25:10, 17
Hes. 10:33Kum 1:32, 33; Yos 3:3, 4
Hes. 10:34Kut 13:21; Ne 9:12; Zb 78:14
Hes. 10:35Zb 132:8
Hes. 10:36Kum 1:10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Hesabu 10:1-36

Hesabu

10 Kisha Yehova akamwambia Musa: 2 “Jitengenezee tarumbeta mbili+ za fedha; zitengeneze kwa kutumia nyundo, nawe uzitumie kuwakusanya watu na kuvunja kambi. 3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, ni lazima Waisraeli wote wakusanyike mbele yako kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 4 Tarumbeta moja tu ikipigwa, ni wakuu peke yao watakaokusanyika mbele yako, yaani, viongozi wa maelfu katika Israeli.+

5 “Mkipiga tarumbeta kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa mashariki+ wanapaswa kuanza safari. 6 Mkipiga tarumbeta mara ya pili kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa kusini+ wanapaswa kuanza safari. Tarumbeta inapaswa kupigwa kwa njia hiyo kila mara kambi moja inapoanza safari.

7 “Mnapowakusanya watu wote, mnapaswa kuzipiga tarumbeta+ kwa mlio usiobadilika-badilika. 8 Wana wa Haruni, makuhani, wanapaswa kuzipiga tarumbeta;+ na hiyo itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote.

9 “Ikiwa maadui wanaowakandamiza watawashambulia katika nchi yenu, mnapaswa kupiga mwito wa vita kwa tarumbeta hizo,+ na Yehova Mungu wenu atawakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.

10 “Pia, katika siku zenu za kushangilia+—wakati wa sherehe zenu+ na mwanzoni mwa miezi yenu—mtazipiga tarumbeta hizo mnapotoa* dhabihu zenu za kuteketezwa+ na dhabihu zenu za ushirika;+ zitanifanya mimi Mungu wenu niwakumbuke. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+

11 Basi katika mwaka wa pili, mwezi wa pili, siku ya 20 ya mwezi huo,+ lile wingu liliinuka kutoka juu ya hema+ la Ushahidi. 12 Kwa hiyo Waisraeli wakaanza kuondoka katika nyika ya Sinai kulingana na utaratibu uliowekwa wa kuondoka,+ na wingu hilo likasimama katika nyika ya Parani.+ 13 Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwao kuondoka kama Yehova alivyokuwa amewaagiza kupitia Musa.+

14 Kwa hiyo kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Yuda liliondoka kwanza kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 15 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Isakari alikuwa Nethaneli+ mwana wa Zuari. 16 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Zabuloni alikuwa Eliabu+ mwana wa Heloni.

17 Hema la ibada lilipofunguliwa,+ wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ waliobeba hema hilo, walianza safari.

18 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 19 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Simeoni alikuwa Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Gadi alikuwa Eliasafu+ mwana wa Deueli.

21 Kisha Wakohathi, waliobeba vyombo vya mahali patakatifu,+ wakaondoka. Hema la ibada lilipaswa kusimamishwa kabla hawajafika.

22 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Efraimu liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elishama+ mwana wa Amihudi. 23 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Manase alikuwa Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Benjamini alikuwa Abidani+ mwana wa Gidioni.

25 Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Dani liliondoka kulingana na vikosi vyake,* nao walikuwa kikosi cha nyuma cha kulinda kambi zote, na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Asheri alikuwa Pagieli+ mwana wa Okrani. 27 Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Naftali alikuwa Ahira+ mwana wa Enani. 28 Huo ndio utaratibu ambao Waisraeli na vikosi vyao walifuata* kila mara walipoanza safari.+

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mmidiani, baba mkwe wake: “Tunaenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’+ Basi twende pamoja,+ nasi tutakutendea mema, kwa sababu Yehova ameahidi kuwapa Waisraeli mambo mema.”+ 30 Lakini akamwambia: “Sitaenda. Nitarudi katika nchi yangu na kwa watu wangu wa ukoo.” 31 Musa akamwambia: “Tafadhali usituache, kwa maana unajua mahali tunapopaswa kupiga kambi nyikani, nawe unaweza kutuonyesha njia.* 32 Ukienda pamoja nasi,+ jambo lolote jema ambalo Yehova atatutendea, bila shaka tutakutendea wewe pia.”

33 Basi wakasafiri kwa siku tatu kutoka kwenye mlima wa Yehova,+ na sanduku+ la agano la Yehova lilisafirishwa mbele yao kwa siku hizo tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.+ 34 Nalo wingu la Yehova+ lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka mahali walipokuwa wamepiga kambi.

35 Kila mara Sanduku hilo lilipoanza kusafirishwa, Musa alisema: “Inuka, Ee Yehova,+ acha maadui wako watawanyike, na wale wanaokuchukia wakimbie kutoka mbele zako.” 36 Na lilipowekwa chini, alisema: “Rudi, Ee Yehova, kwa maelfu yasiyohesabika* ya Waisraeli.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki