Methali
5 Mwanangu, sikiliza hekima yangu.
Sikiliza kwa makini* utambuzi wangu,+
2 Ili uweze kuulinda uwezo wako wa kufikiri
Na kuulinda ujuzi kwa midomo yako.+
3 Kwa maana midomo ya mwanamke aliyepotoka* inadondoka kama sega la asali,+
Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+
4 Lakini mwishowe ni mchungu kama pakanga+
Na mwenye makali kama upanga unaokata kwa pande zote mbili.+
5 Miguu yake hushuka kwenye kifo.
Hatua zake huongoza moja kwa moja Kaburini.*
6 Hakazii fikira kijia cha uzima.
Huyumbayumba katika njia yake, lakini hajui inakoelekea.
7 Sasa, wanangu, nisikilizeni
Nanyi msiache ninayosema.
8 Kaeni mbali naye;
Msiukaribie mlango wa nyumba yake,+
9 Ili msiwape wengine heshima yenu+
Wala kuvuna miaka ya ukatili;+
10 Ili wageni wasimalize mali* zenu+
Na vitu mlivyopata kwa jasho viende katika nyumba ya mgeni.
11 La sivyo, mtalia kwa uchungu mwishoni mwa maisha yenu
Nyama na mwili wenu vitakapodhoofika+
12 Nanyi mseme: “Jinsi nilivyochukia nidhamu!
Jinsi moyo wangu ulivyodharau karipio!
13 Sikusikiliza sauti ya wakufunzi wangu
Wala kuwasikiliza kwa makini walimu wangu.
16 Je, chemchemi zako zitawanywe nje,
Na vijito vyako vya maji katika viwanja vya jiji?+
17 Na yawe yako peke yako,
Wala si ya wageni pamoja nawe.+
Matiti yake na yakuridhishe* nyakati zote.
Upendo wake na ukusisimue daima.+
20 Basi mwanangu, kwa nini usisimuliwe na mwanamke aliyepotoka*
21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;
Yeye huvichunguza vijia vyake vyote.+
22 Mwovu hunaswa na makosa yake mwenyewe,
Naye atashikwa na kamba za dhambi yake mwenyewe.+
23 Atakufa kwa sababu ya utovu wa nidhamu
Na kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake uliopita kiasi.