Zaburi
115 Usitutukuze sisi, Ee Yehova, usitutukuze sisi,*
Bali litukuze jina lako+
Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.+
2 Kwa nini mataifa yaseme:
“Yuko wapi Mungu wao?”+
3 Mungu wetu yuko mbinguni;
Hufanya lolote apendalo.
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
5 Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona;
6 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia;
Zina pua, lakini haziwezi kunusa;
7 Zina mikono, lakini haziwezi kugusa;
Zina miguu, lakini haziwezi kutembea;+
Hazitoi sauti yoyote kwa koo zake.+
10 Ee nyumba ya Haruni,+ mtumainini Yehova;
—Yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.
13 Atawabariki wale wanaomwogopa Yehova,
Wadogo kwa wakubwa.
18 Lakini sisi tutamsifu Yah
Kuanzia sasa mpaka milele.
Msifuni Yah!*