Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Hesabu—Yaliyomo

      • Sheria kuhusu dhabihu (1-21)

        • Sheria zilezile kwa wenyeji na wageni (15, 16)

      • Dhabihu kwa ajili ya dhambi zilizofanywa bila kukusudia (22-29)

      • Adhabu kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kimakusudi (30, 31)

      • Aliyevunja Sabato auawa (32-36)

      • Mavazi yawe na upindo wa nyuzinyuzi (37-41)

Hesabu 15:2

Marejeo

  • +Mwa 15:18

Hesabu 15:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Law 1:2, 3
  • +Law 7:16; 22:18, 19, 21
  • +Law 23:4; Hes 28:16; 29:1; Kum 16:13, 16
  • +Law 1:9

Hesabu 15:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Sehemu ya kumi ya efa ilikuwa sawa na lita 2.2 au kilogramu 1.3 hivi. Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Hini ilikuwa sawa na lita 3.67. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Kut 29:40; Law 2:1, 11

Hesabu 15:5

Marejeo

  • +Hes 28:6, 7, 11, 14

Hesabu 15:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Hesabu 15:8

Marejeo

  • +Law 1:3
  • +Law 7:16
  • +Law 3:1, 3; 7:11

Hesabu 15:9

Marejeo

  • +Law 6:14; Hes 28:11, 12; 29:6

Hesabu 15:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Hes 28:11, 14

Hesabu 15:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Hesabu 15:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Kut 12:49; Law 24:22; Hes 9:14

Hesabu 15:15

Marejeo

  • +Law 19:34

Hesabu 15:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “maamuzi yaleyale ya hukumu.”

Hesabu 15:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mkate wowote wa.”

Marejeo

  • +Yos 5:11, 12

Hesabu 15:20

Marejeo

  • +Kut 23:19; Law 2:14; Hes 18:8, 12; Kum 26:1, 2; Met 3:9

Hesabu 15:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “inayomtuliza.”

Marejeo

  • +Hes 15:8-10
  • +Hes 28:15

Hesabu 15:25

Marejeo

  • +Law 4:20; Ebr 2:17; 1Yo 2:1, 2

Hesabu 15:27

Marejeo

  • +Law 4:27, 28

Hesabu 15:28

Marejeo

  • +Law 4:32, 35

Hesabu 15:29

Marejeo

  • +Kut 12:49; Law 24:22; Hes 9:14; 15:15

Hesabu 15:30

Marejeo

  • +Kut 21:14; Kum 17:12; Ebr 10:26, 27

Hesabu 15:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Kosa lake litakuwa juu ya kichwa chake.”

Marejeo

  • +Ebr 10:28
  • +Eze 18:20

Hesabu 15:32

Marejeo

  • +Kut 20:9, 10; 35:2; Kum 5:13, 14

Hesabu 15:34

Marejeo

  • +Law 24:11, 12

Hesabu 15:35

Marejeo

  • +Kut 31:14
  • +Law 24:14

Hesabu 15:38

Marejeo

  • +Kum 22:12; Mt 23:5

Hesabu 15:39

Marejeo

  • +Kum 11:18
  • +Kut 34:15

Hesabu 15:40

Marejeo

  • +Law 11:44; Ro 12:1; 1Pe 1:15

Hesabu 15:41

Marejeo

  • +Mwa 17:8; Kut 29:45; Law 25:38
  • +Kut 3:15; 6:2, 3

Jumla

Hes. 15:2Mwa 15:18
Hes. 15:3Law 1:2, 3
Hes. 15:3Law 7:16; 22:18, 19, 21
Hes. 15:3Law 23:4; Hes 28:16; 29:1; Kum 16:13, 16
Hes. 15:3Law 1:9
Hes. 15:4Kut 29:40; Law 2:1, 11
Hes. 15:5Hes 28:6, 7, 11, 14
Hes. 15:8Law 1:3
Hes. 15:8Law 7:16
Hes. 15:8Law 3:1, 3; 7:11
Hes. 15:9Law 6:14; Hes 28:11, 12; 29:6
Hes. 15:10Hes 28:11, 14
Hes. 15:14Kut 12:49; Law 24:22; Hes 9:14
Hes. 15:15Law 19:34
Hes. 15:19Yos 5:11, 12
Hes. 15:20Kut 23:19; Law 2:14; Hes 18:8, 12; Kum 26:1, 2; Met 3:9
Hes. 15:24Hes 15:8-10
Hes. 15:24Hes 28:15
Hes. 15:25Law 4:20; Ebr 2:17; 1Yo 2:1, 2
Hes. 15:27Law 4:27, 28
Hes. 15:28Law 4:32, 35
Hes. 15:29Kut 12:49; Law 24:22; Hes 9:14; 15:15
Hes. 15:30Kut 21:14; Kum 17:12; Ebr 10:26, 27
Hes. 15:31Ebr 10:28
Hes. 15:31Eze 18:20
Hes. 15:32Kut 20:9, 10; 35:2; Kum 5:13, 14
Hes. 15:34Law 24:11, 12
Hes. 15:35Kut 31:14
Hes. 15:35Law 24:14
Hes. 15:38Kum 22:12; Mt 23:5
Hes. 15:39Kum 11:18
Hes. 15:39Kut 34:15
Hes. 15:40Law 11:44; Ro 12:1; 1Pe 1:15
Hes. 15:41Mwa 17:8; Kut 29:45; Law 25:38
Hes. 15:41Kut 3:15; 6:2, 3
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Hesabu 15:1-41

Hesabu

15 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 2 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Hatimaye mtakapoingia katika nchi ninayowapa mwishi ndani yake,+ 3 na kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto kutoka kati ya mifugo au kundi—iwe ni dhabihu ya kuteketezwa+ au dhabihu ya kutimiza nadhiri ya pekee au toleo la hiari+ au dhabihu mnayotoa wakati wa sherehe zenu za majira,+ ili kumtolea Yehova harufu inayompendeza*+— 4 ni lazima pia mtu anayetoa dhabihu yake amtolee Yehova sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja* ya unga laini+ uliochanganywa na robo ya hini* ya mafuta ili iwe toleo la nafaka. 5 Pia mnapaswa kutoa robo ya kipimo cha hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji; mtaitoa pamoja na dhabihu ya kuteketezwa+ au pamoja na dhabihu ya kila mwanakondoo dume. 6 Au mtatoa kondoo dume pamoja na sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa moja ya unga laini uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka. 7 Nanyi mnapaswa kutoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji lenye harufu inayompendeza* Yehova.

8 “‘Lakini mkimtolea Yehova mnyama dume kutoka katika mifugo yenu ili awe dhabihu ya kuteketezwa+ au dhabihu ya kutimiza nadhiri ya pekee+ au dhabihu za ushirika,+ 9 mnapaswa kumtoa mnyama dume huyo pamoja na sehemu tatu za kumi za kipimo cha efa moja ya unga laini uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka.+ 10 Mnapaswa pia kutoa nusu ya hini ya divai ili iwe toleo la kinywaji+ linalochomwa kwa moto lenye harufu inayompendeza* Yehova. 11 Hivyo ndivyo mnavyopaswa kumtoa kila ng’ombe dume au kila kondoo dume au kila mwanakondoo dume au mbuzi dume. 12 Haidhuru mnatoa wanyama wangapi, mnapaswa kutoa vitu hivyo pamoja na kila mnyama mnayemtoa, kulingana na idadi yao. 13 Hivyo ndivyo kila Mwisraeli mwenyeji anavyopaswa kutoa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.

14 “‘Ikiwa mgeni anayeishi nanyi au mtu mwingine ambaye ameishi pamoja nanyi kwa muda mrefu atatoa pia dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova, anapaswa kufanya kama mnavyofanya.+ 15 Ninyi pamoja na mgeni anayeishi miongoni mwenu mtafuata sheria zilezile. Itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyenu vyote. Ninyi pamoja na mgeni mtakuwa sawa mbele za Yehova.+ 16 Ninyi na mgeni anayeishi miongoni mwenu mtafuata sheria zilezile na amri zilezile.’”*

17 Yehova akaendelea kumwambia Musa, 18 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka 19 nanyi mle chakula chochote cha* nchi hiyo,+ mnapaswa kumtolea Yehova kiasi fulani kama mchango. 20 Mtatoa mchango wa mazao ya kwanza+ ya mikate ya mviringo iliyookwa kwa unga wenu ambao haujakobolewa. Mtautoa kama mchango unaotoka katika uwanja wa kupuria nafaka. 21 Baadhi ya mazao ya kwanza ya unga wenu ambao haujakobolewa mtamtolea Yehova mchango katika vizazi vyenu vyote.

22 “‘Sasa mkifanya kosa, nanyi mkose kushika amri hizi zote ambazo mimi, Yehova, nimempa Musa, 23 mambo yote ambayo mimi, Yehova, nimewaamuru ninyi kupitia Musa katika vizazi vyenu tangu siku ambayo mimi Yehova niliamuru, 24 na ikiwa kosa hilo lilifanywa bila kukusudia na bila kusanyiko lote kujua, basi ni lazima kusanyiko lote litoe dhabihu ya kuteketezwa ya ng’ombe dume mchanga ili iwe harufu inayompendeza* Yehova, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji kulingana na utaratibu wa kawaida,+ na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+ 25 Kuhani atatoa dhabihu ya kufunika dhambi ya kusanyiko lote la Waisraeli, nao watasamehewa,+ kwa sababu lilikuwa kosa, nao walimletea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto na kuleta dhabihu yao ya dhambi mbele za Yehova kwa ajili ya kosa lao. 26 Kusanyiko lote la Waisraeli pamoja na wageni wanaokaa miongoni mwao watasamehewa kosa hilo kwa sababu watu wote walihusika.

27 “‘Mtu yeyote akifanya dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi.+ 28 Kisha kuhani atatoa dhabihu ili mtu aliyetenda dhambi mbele za Yehova bila kukusudia asamehewe dhambi yake, yaani, atamtolea dhabihu ya kufunika dhambi yake, na mtu huyo atasamehewa.+ 29 Waisraeli wenyeji na pia wageni wanaoishi miongoni mwao watafuata sheria zilezile zinazomhusu mtu anayetenda kosa bila kukusudia.+

30 “‘Lakini mtu anayetenda kosa kimakusudi,+ awe ni mwenyeji au mgeni, anamkufuru Yehova, naye lazima auawe. 31 Kwa kuwa amedharau neno la Yehova na kuvunja amri yake, ni lazima mtu huyo auawe.+ Ataadhibiwa kwa sababu ya kosa lake.’”*+

32 Waisraeli walipokuwa nyikani, walimkuta mtu fulani akiokota kuni siku ya Sabato.+ 33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni na Waisraeli wote. 34 Wakamtia kifungoni+ kwa sababu sheria haikusema waziwazi mtu huyo afanyiwe nini.

35 Basi Yehova akamwambia Musa: “Ni lazima mtu huyo auawe,+ Waisraeli wote watampiga mawe nje ya kambi.”+ 36 Basi Waisraeli wote wakamtoa nje ya kambi, wakampiga mawe na kumuua, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

37 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 38 “Waambie Waisraeli wajitengenezee upindo wa nyuzinyuzi kwenye ncha za mavazi yao katika vizazi vyao vyote, nao watashona uzi wa bluu juu ya upindo huo wa nyuzinyuzi.+ 39 ‘Mnapaswa kutengeneza upindo huo wa nyuzinyuzi ili muuone na kukumbuka amri zote za Yehova na kuzishika.+ Msifuate mioyo yenu na macho yenu, ambayo yanawaongoza kwenye ukahaba wa kiroho.+ 40 Upindo huo utawasaidia kukumbuka, nanyi mtashika amri zangu zote na kuwa watakatifu kwangu mimi Mungu wenu.+ 41 Mimi ni Yehova Mungu wenu, niliyewatoa nchini Misri ili nijithibitishe kuwa Mungu wenu.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki