Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 38
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Gogu kushambulia Israeli (1-16)

      • Hasira ya Yehova dhidi ya Gogu (17-23)

        • ‘Mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova’ (23)

Ezekieli 38:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mkuu wa wakuu.”

Marejeo

  • +Eze 38:15
  • +Isa 66:19; Eze 27:13; 32:26
  • +Eze 39:1

Ezekieli 38:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mkuu wa wakuu.”

Ezekieli 38:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.

Marejeo

  • +2Fa 19:20, 28; Eze 29:3, 4; 39:2
  • +Eze 38:15

Ezekieli 38:5

Marejeo

  • +1Nya 1:8

Ezekieli 38:6

Marejeo

  • +Mwa 10:2, 3; Eze 27:14
  • +Eze 39:2

Ezekieli 38:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mlinzi.”

Ezekieli 38:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Utaitwa.”

Marejeo

  • +Yer 23:5, 6; Eze 28:25, 26; 34:25

Ezekieli 38:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “eneo lililo wazi la mashambani.”

Marejeo

  • +Kut 15:9

Ezekieli 38:12

Marejeo

  • +Yer 33:12
  • +Zek 10:8
  • +Isa 60:5; 61:6

Ezekieli 38:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”

Marejeo

  • +Eze 27:22
  • +Eze 27:15
  • +Eze 27:25

Ezekieli 38:14

Marejeo

  • +Eze 38:8

Ezekieli 38:15

Marejeo

  • +Eze 39:2
  • +Sef 3:8

Ezekieli 38:16

Marejeo

  • +Yoe 3:2
  • +Kut 14:4; 2Fa 19:17-19; Zb 83:17, 18; Eze 39:21

Ezekieli 38:18

Marejeo

  • +Yoe 3:16; Nah 1:2; Zek 2:8

Ezekieli 38:20

Marejeo

  • +Nah 1:5

Ezekieli 38:21

Marejeo

  • +2Nya 20:23; Hag 2:22; Zek 14:13

Ezekieli 38:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nitamhukumu.”

Marejeo

  • +Zek 14:12
  • +Kut 9:22; Yos 10:11
  • +Isa 30:30
  • +Mwa 19:24
  • +Yer 25:31

Jumla

Eze. 38:2Eze 38:15
Eze. 38:2Isa 66:19; Eze 27:13; 32:26
Eze. 38:2Eze 39:1
Eze. 38:42Fa 19:20, 28; Eze 29:3, 4; 39:2
Eze. 38:4Eze 38:15
Eze. 38:51Nya 1:8
Eze. 38:6Mwa 10:2, 3; Eze 27:14
Eze. 38:6Eze 39:2
Eze. 38:8Yer 23:5, 6; Eze 28:25, 26; 34:25
Eze. 38:11Kut 15:9
Eze. 38:12Yer 33:12
Eze. 38:12Zek 10:8
Eze. 38:12Isa 60:5; 61:6
Eze. 38:13Eze 27:22
Eze. 38:13Eze 27:15
Eze. 38:13Eze 27:25
Eze. 38:14Eze 38:8
Eze. 38:15Eze 39:2
Eze. 38:15Sef 3:8
Eze. 38:16Yoe 3:2
Eze. 38:16Kut 14:4; 2Fa 19:17-19; Zb 83:17, 18; Eze 39:21
Eze. 38:18Yoe 3:16; Nah 1:2; Zek 2:8
Eze. 38:20Nah 1:5
Eze. 38:212Nya 20:23; Hag 2:22; Zek 14:13
Eze. 38:22Zek 14:12
Eze. 38:22Kut 9:22; Yos 10:11
Eze. 38:22Isa 30:30
Eze. 38:22Mwa 19:24
Eze. 38:22Yer 25:31
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 38:1-23

Ezekieli

38 Neno la Yehova likanijia tena likisema: 2 “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako dhidi ya Gogu wa nchi ya Magogu,+ kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali,+ na utabiri dhidi yake.+ 3 Sema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama, niko dhidi yako, ewe Gogu, kiongozi mkuu* wa Mesheki na Tubali. 4 Nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako+ na kukutoa pamoja na jeshi lako lote,+ farasi na wapanda farasi, wote wakiwa wamevaa mavazi ya kifahari, kusanyiko kubwa sana lenye ngao kubwa na ngao ndogo,* wote wakiwa na mapanga; 5 Uajemi, Ethiopia, na Putu+ wako pamoja nao, wote wakiwa na ngao ndogo na kofia; 6 Gomeri na wanajeshi wake wote, watu wa nyumba ya Togarma+ kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, pamoja na wanajeshi wake wote—mataifa mengi yako pamoja nawe.+

7 “‘“Uwe tayari, ujitayarishe, wewe pamoja na majeshi yako yote yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe utakuwa kamanda* wao.

8 “‘“Utakaziwa fikira* baada ya siku nyingi. Katika miaka ya mwisho utaishambulia nchi ambayo watu wake wamerudishwa kutoka kwenye uharibifu wa upanga, waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa mengi, na kuletwa kwenye milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imebaki ukiwa. Wakaaji wa nchi hii walirudishwa kutoka katika mataifa, na wote wanakaa kwa usalama.+ 9 Utawashambulia kama dhoruba nawe utaifunika nchi kama mawingu, wewe na wanajeshi wako wote na mataifa mengi pamoja nawe.”’

10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Siku hiyo mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utapanga njama ya uovu. 11 Utasema: “Nitaivamia nchi yenye vijiji visivyo na ulinzi.*+ Nitawashambulia wale wanaokaa kwa usalama, bila usumbufu, wote wanaoishi katika vijiji visivyolindwa na ukuta, makomeo, au malango.” 12 Ili kupora na kuchukua nyara nyingi, ili kushambulia maeneo yaliyoharibiwa ambayo sasa yanakaliwa na watu+ waliokusanywa kutoka katika mataifa,+ ambao wanajikusanyia utajiri na mali,+ wale wanaoishi katikati ya dunia.

13 “‘Sheba+ na Dedani,+ wafanyabiashara wa Tarshishi+ na mashujaa* wake wote watakuuliza: “Je, unavamia ili upore na kupata nyara nyingi? Je, umekusanya majeshi yako ili kubeba fedha na dhahabu, kuchukua utajiri na mali, ili kuteka nyara nyingi sana?”’

14 “Basi tabiri, mwana wa binadamu, nawe umwambie Gogu, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Siku ambayo watu wangu Waisraeli watakapokuwa wakiishi kwa usalama, je, hutajua jambo hilo?+ 15 Utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini,+ wewe pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, jeshi kubwa sana.+ 16 Kama mawingu yanayoifunika nchi, utawashambulia watu wangu Waisraeli. Katika kipindi cha mwisho cha zile siku, nitakuleta uishambulie nchi yangu+ ili mataifa yanijue nitakapojitakasa mwenyewe kupitia wewe mbele ya macho yao, ewe Gogu.”’+

17 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Je, wewe si yuleyule niliyesema kumhusu katika siku za zamani kupitia watumishi wangu manabii wa Israeli, waliotabiri kwa miaka mingi kwamba utaletwa ili kuwashambulia?’

18 “‘Siku hiyo, siku ambayo Gogu ataishambulia nchi ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ghadhabu yangu kali itawaka.+ 19 Kwa bidii yangu, kwa moto wa ghadhabu yangu, nitazungumza; na siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la ardhi katika nchi ya Israeli. 20 Kwa sababu yangu, samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa mwituni, wanyama wote wanaotambaa juu ya nchi, na wanadamu wote walio duniani watatetemeka, nayo milima itaangushwa chini,+ na miamba itaanguka, na kila ukuta utaporomoka.’

21 “‘Nitauita upanga umshambulie kwenye milima yangu yote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Upanga wa kila mtu utamshambulia ndugu yake mwenyewe.+ 22 Nitamletea hukumu yangu* kwa ugonjwa hatari+ na kwa umwagaji wa damu; nami nitaleta dhidi yake mvua kubwa ya mafuriko na mawe ya mvua+ na moto+ na kiberiti+ na dhidi ya wanajeshi wake na dhidi ya mataifa mengi yaliyo pamoja naye.+ 23 Nami hakika nitajitukuza na kujitakasa na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki