Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 19
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Kwenye Mlima Sinai (1-25)

        • Waisraeli watakuwa ufalme wa makuhani (5, 6)

        • Watu watakaswa ili wakutane na Mungu (14, 15)

Kutoka 19:2

Marejeo

  • +Kut 17:1
  • +Kut 3:1, 12

Kutoka 19:3

Marejeo

  • +Mdo 7:38

Kutoka 19:4

Marejeo

  • +Kum 4:34
  • +Kum 32:11, 12; Isa 63:9

Kutoka 19:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mali yangu ninayothamini sana.”

Marejeo

  • +1Fa 8:53; Zb 135:4
  • +Kum 10:14

Kutoka 19:6

Marejeo

  • +Law 11:44; Kum 7:6; 1Pe 2:9; Ufu 5:9, 10

Kutoka 19:7

Marejeo

  • +Kut 24:3

Kutoka 19:8

Marejeo

  • +Kut 24:7; Yos 24:24

Kutoka 19:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Labda angechomwa kwa mkuki.

Marejeo

  • +Ebr 12:20
  • +Kut 20:18

Kutoka 19:14

Marejeo

  • +Kut 19:10

Kutoka 19:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Msimkaribie mwanamke.”

Kutoka 19:16

Marejeo

  • +Kum 4:11; 1Fa 8:12; Zb 97:2
  • +Ebr 12:18-21

Kutoka 19:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kalibu.”

Marejeo

  • +Kut 24:17; Kum 4:11, 12; 2Nya 7:1-3
  • +Zb 68:8

Kutoka 19:20

Marejeo

  • +Kut 24:12

Kutoka 19:22

Marejeo

  • +Law 10:1, 2; 1Nya 13:10

Kutoka 19:23

Marejeo

  • +Kut 19:12

Kutoka 19:24

Marejeo

  • +Hes 16:19, 35

Jumla

Kut. 19:2Kut 17:1
Kut. 19:2Kut 3:1, 12
Kut. 19:3Mdo 7:38
Kut. 19:4Kum 4:34
Kut. 19:4Kum 32:11, 12; Isa 63:9
Kut. 19:51Fa 8:53; Zb 135:4
Kut. 19:5Kum 10:14
Kut. 19:6Law 11:44; Kum 7:6; 1Pe 2:9; Ufu 5:9, 10
Kut. 19:7Kut 24:3
Kut. 19:8Kut 24:7; Yos 24:24
Kut. 19:13Ebr 12:20
Kut. 19:13Kut 20:18
Kut. 19:14Kut 19:10
Kut. 19:16Kum 4:11; 1Fa 8:12; Zb 97:2
Kut. 19:16Ebr 12:18-21
Kut. 19:18Kut 24:17; Kum 4:11, 12; 2Nya 7:1-3
Kut. 19:18Zb 68:8
Kut. 19:20Kut 24:12
Kut. 19:22Law 10:1, 2; 1Nya 13:10
Kut. 19:23Kut 19:12
Kut. 19:24Hes 16:19, 35
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 19:1-25

Kutoka

19 Katika mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kutoka nchini Misri, siku ileile, walifika katika nyika ya Sinai. 2 Waliondoka Refidimu+ wakafika katika nyika ya Sinai na kupiga kambi nyikani. Waisraeli walipiga kambi huko mbele ya mlima.+

3 Kisha Musa akapanda mlimani kwa Mungu wa kweli, naye Yehova akamwita kutoka mlimani,+ akamwambia: “Hivi ndivyo utakavyoiambia nyumba ya Yakobo na kuwaambia Waisraeli, 4 ‘Mmejionea wenyewe mambo niliyowatendea Wamisri,+ ili niwabebe juu ya mabawa ya tai na kuwaleta kwangu.+ 5 Sasa ikiwa mtaitii kabisa sauti yangu na kushika agano langu, hakika mtakuwa mali yangu ya pekee* kati ya mataifa yote,+ kwa maana dunia yote ni mali yangu.+ 6 Mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’+ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”

7 Basi Musa akaenda na kuwaita wazee wote wa Waisraeli na kuwaambia maneno hayo yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru.+ 8 Kisha watu wote wakasema pamoja: “Mambo yote ambayo Yehova amesema, tuko tayari kufanya.”+ Mara moja Musa akamwambia Yehova maneno hayo ambayo watu walisema. 9 Na Yehova akamwambia Musa: “Tazama! nitakujia katika wingu lenye giza, ili watu wasikie ninapozungumza nawe na ili wakuamini wewe pia sikuzote.” Kisha Musa akamwambia Yehova maneno ambayo watu walisema.

10 Halafu Yehova akamwambia Musa: “Nenda uwatakase watu leo na kesho, nao lazima wafue nguo zao. 11 Nao lazima wawe tayari kwa ajili ya siku ya tatu, kwa sababu katika siku ya tatu mimi Yehova nitashuka juu ya Mlima Sinai mbele ya watu wote. 12 Ni lazima uwawekee watu mipaka kuzunguka mlima huu na uwaambie, ‘Jihadharini msipande mlimani wala kugusa ukingo wake. Yeyote atakayeugusa mlima huu hakika atauawa. 13 Mkono wa yeyote usimguse, atapigwa mawe au kuchomwa kwa silaha.* Awe ni mnyama au mwanadamu, hataishi.’+ Lakini pembe ya kondoo dume+ ikipigwa watu wanaweza kuukaribia mlima.”

14 Kisha Musa akashuka kutoka mlimani, akaenda kwa watu, akaanza kuwatakasa, nao wakafua nguo zao.+ 15 Akawaambia: “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Msifanye ngono.”*

16 Asubuhi, siku ya tatu, kulikuwa na ngurumo na radi, na kulikuwa na wingu zito+ mlimani na sauti kubwa sana ya pembe, na watu wote kambini wakaanza kutetemeka.+ 17 Sasa Musa akawatoa watu nje ya kambi ili wakutane na Mungu wa kweli, nao wakasimama mahali pao chini ya mlima. 18 Mlima Sinai ulifuka moshi kila mahali, kwa sababu Yehova alishuka juu yake katika moto;+ na moshi huo ulikuwa ukipaa kama moshi wa tanuru,* na mlima wote ulikuwa ukitetemeka kwa nguvu sana.+ 19 Sauti ya pembe ilipozidi kuongezeka zaidi na zaidi, Musa akaongea, na sauti ya Mungu wa kweli ikamjibu.

20 Kwa hiyo Yehova akashuka juu ya kilele cha Mlima Sinai. Kisha Yehova akamwita Musa apande juu mlimani, naye Musa akapanda mlimani.+ 21 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Shuka chini ukawaonye watu wasijaribu kuvuka mpaka kuja kunitazama mimi, Yehova, la sivyo wengi wao wataangamia. 22 Nao makuhani wanaonikaribia mimi Yehova kwa ukawaida, wanapaswa kujitakasa, ili mimi, Yehova, nisiwaangamize.”+ 23 Basi Musa akamwambia Yehova: “Watu hawawezi kuukaribia Mlima Sinai kwa sababu tayari ulituonya, uliponiambia, ‘Weka mipaka kuzunguka mlima huu, ili uwe mtakatifu.’”+ 24 Hata hivyo, Yehova akamwambia: “Nenda, shuka chini, na urudi juu, wewe pamoja na Haruni, lakini usiwaruhusu makuhani na watu wavuke mpaka na kunikaribia mimi Yehova, ili nisiwaangamize.”+ 25 Basi Musa akashuka na kuwaambia watu maneno hayo.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki