Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 32
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Hesabu—Yaliyomo

      • Waliobaki upande wa mashariki wa Yordani (1-42)

Hesabu 32:1

Marejeo

  • +Hes 26:7
  • +Hes 26:18
  • +Hes 21:32

Hesabu 32:3

Marejeo

  • +Hes 21:26
  • +Hes 33:47
  • +Hes 32:37, 38

Hesabu 32:4

Marejeo

  • +Hes 21:23, 24; Kum 2:24
  • +Kum 2:35

Hesabu 32:8

Marejeo

  • +Hes 13:31; Yos 14:7, 8

Hesabu 32:9

Marejeo

  • +Hes 13:23; Kum 1:24
  • +Hes 13:32; Kum 1:26-28

Hesabu 32:10

Marejeo

  • +Zb 95:11; Eze 20:15; Ebr 3:18

Hesabu 32:11

Marejeo

  • +Hes 14:29, 30; Kum 2:14
  • +Mwa 13:14, 15; 26:3; 28:13

Hesabu 32:12

Marejeo

  • +Hes 13:30
  • +Yos 19:49
  • +Hes 14:24; Kum 1:34-38; Yos 14:8

Hesabu 32:13

Marejeo

  • +Hes 14:33; Kum 29:5; Yos 5:6; Zb 95:10; Mdo 13:18
  • +Hes 26:63, 64; Kum 2:14; 1Ko 10:5; Ebr 3:17

Hesabu 32:17

Marejeo

  • +Kum 3:18; Yos 4:12

Hesabu 32:18

Marejeo

  • +Yos 22:1, 4

Hesabu 32:19

Marejeo

  • +Hes 32:33; Yos 12:1; 13:8

Hesabu 32:20

Marejeo

  • +Yos 4:13

Hesabu 32:21

Marejeo

  • +Zb 78:55

Hesabu 32:22

Marejeo

  • +Yos 11:23; 18:1; Zb 44:2
  • +Yos 22:4, 9
  • +Kum 3:19, 20; Yos 1:14, 15; 13:8

Hesabu 32:24

Marejeo

  • +Hes 32:16, 34-38

Hesabu 32:26

Marejeo

  • +Yos 1:12-14

Hesabu 32:27

Marejeo

  • +Yos 4:12

Hesabu 32:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ukoo wa upande wa baba.

Hesabu 32:29

Marejeo

  • +Yos 13:15, 24

Hesabu 32:32

Marejeo

  • +Yos 4:13

Hesabu 32:33

Marejeo

  • +Kum 3:12
  • +Yos 22:7
  • +Hes 21:23, 24; Kum 2:31
  • +Kum 3:4

Hesabu 32:34

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wakajenga upya.”

Marejeo

  • +Hes 33:45; Yos 13:15, 17
  • +Hes 32:3, 4
  • +Kum 2:36; Yos 12:1, 2

Hesabu 32:35

Marejeo

  • +Hes 21:32
  • +Amu 8:11

Hesabu 32:36

Marejeo

  • +Hes 32:3, 4
  • +Yos 13:27, 28

Hesabu 32:37

Marejeo

  • +Hes 21:26
  • +Hes 32:3, 4
  • +Yos 13:15, 19

Hesabu 32:38

Marejeo

  • +Hes 32:3, 4
  • +Yos 13:15, 17

Hesabu 32:39

Marejeo

  • +Hes 26:29

Hesabu 32:40

Marejeo

  • +Kum 3:13; Yos 13:31; 17:1

Hesabu 32:41

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Vijiji vya Mahema vya Yairi.”

Marejeo

  • +Kum 3:14; Yos 13:29, 30

Jumla

Hes. 32:1Hes 26:7
Hes. 32:1Hes 26:18
Hes. 32:1Hes 21:32
Hes. 32:3Hes 21:26
Hes. 32:3Hes 33:47
Hes. 32:3Hes 32:37, 38
Hes. 32:4Hes 21:23, 24; Kum 2:24
Hes. 32:4Kum 2:35
Hes. 32:8Hes 13:31; Yos 14:7, 8
Hes. 32:9Hes 13:23; Kum 1:24
Hes. 32:9Hes 13:32; Kum 1:26-28
Hes. 32:10Zb 95:11; Eze 20:15; Ebr 3:18
Hes. 32:11Hes 14:29, 30; Kum 2:14
Hes. 32:11Mwa 13:14, 15; 26:3; 28:13
Hes. 32:12Hes 13:30
Hes. 32:12Yos 19:49
Hes. 32:12Hes 14:24; Kum 1:34-38; Yos 14:8
Hes. 32:13Hes 14:33; Kum 29:5; Yos 5:6; Zb 95:10; Mdo 13:18
Hes. 32:13Hes 26:63, 64; Kum 2:14; 1Ko 10:5; Ebr 3:17
Hes. 32:17Kum 3:18; Yos 4:12
Hes. 32:18Yos 22:1, 4
Hes. 32:19Hes 32:33; Yos 12:1; 13:8
Hes. 32:20Yos 4:13
Hes. 32:21Zb 78:55
Hes. 32:22Yos 11:23; 18:1; Zb 44:2
Hes. 32:22Yos 22:4, 9
Hes. 32:22Kum 3:19, 20; Yos 1:14, 15; 13:8
Hes. 32:24Hes 32:16, 34-38
Hes. 32:26Yos 1:12-14
Hes. 32:27Yos 4:12
Hes. 32:29Yos 13:15, 24
Hes. 32:32Yos 4:13
Hes. 32:33Kum 3:12
Hes. 32:33Yos 22:7
Hes. 32:33Hes 21:23, 24; Kum 2:31
Hes. 32:33Kum 3:4
Hes. 32:34Hes 33:45; Yos 13:15, 17
Hes. 32:34Hes 32:3, 4
Hes. 32:34Kum 2:36; Yos 12:1, 2
Hes. 32:35Hes 21:32
Hes. 32:35Amu 8:11
Hes. 32:36Hes 32:3, 4
Hes. 32:36Yos 13:27, 28
Hes. 32:37Hes 21:26
Hes. 32:37Hes 32:3, 4
Hes. 32:37Yos 13:15, 19
Hes. 32:38Hes 32:3, 4
Hes. 32:38Yos 13:15, 17
Hes. 32:39Hes 26:29
Hes. 32:40Kum 3:13; Yos 13:31; 17:1
Hes. 32:41Kum 3:14; Yos 13:29, 30
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Hesabu 32:1-42

Hesabu

32 Sasa wana wa Rubeni+ na wana wa Gadi+ walikuwa na mifugo mingi sana, wakaona kwamba eneo la Yazeri+ na eneo la Gileadi yalikuwa maeneo mazuri kwa mifugo. 2 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakaja kwa Musa, kuhani Eleazari, na wakuu wa Waisraeli na kuwaambia hivi: 3 “Atarothi, Diboni, Yazeri, Nimra, Heshboni,+ Eleale, Sebamu, Nebo,+ na Beoni,+ 4 maeneo ambayo Yehova aliyashinda mbele ya Waisraeli,+ ni maeneo mazuri kwa mifugo, nasi watumishi wenu tuna mifugo mingi.”+ 5 Wakaendelea kusema, “Ikiwa sisi watumishi wenu tumepata kibali machoni penu, tupeni maeneo haya tuyamiliki. Msituvushe ng’ambo ya Mto Yordani.”

6 Lakini Musa akawaambia hivi wana wa Gadi na wana wa Rubeni: “Je, ndugu zenu wataenda vitani huku ninyi mkiendelea kukaa hapa? 7 Kwa nini muwavunje moyo Waisraeli wasivuke kuingia katika nchi ambayo kwa hakika Yehova atawapa? 8 Hivyo ndivyo baba zenu walivyofanya nilipowatuma kutoka Kadesh-barnea wakaione ile nchi.+ 9 Walipofika kwenye Bonde la Eshkoli+ na kuiona nchi hiyo, waliwavunja moyo Waisraeli wasiingie katika nchi ambayo Yehova angewapa.+ 10 Yehova aliwaka hasira siku hiyo na kuapa hivi:+ 11 ‘Wanaume waliotoka Misri wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi hawataiona nchi+ ambayo niliapa kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo,+ kwa sababu hawakunifuata kwa moyo wote— 12 isipokuwa Kalebu+ mwana wa Yefune, Mkenizi, na Yoshua+ mwana wa Nuni, kwa sababu wamenifuata mimi Yehova kwa moyo wote.’+ 13 Basi hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Waisraeli naye akawafanya watangetange nyikani kwa miaka 40,+ mpaka kizazi chote kilichokuwa kikifanya maovu machoni pa Yehova kilipoangamia.+ 14 Na sasa ninyi mmekuwa kama baba zenu, kundi la watenda dhambi wanaozidisha hasira kali ya Yehova dhidi ya Waisraeli. 15 Mkigeuka na kuacha kumfuata, kwa hakika atawaacha tena watu hawa nyikani, nanyi mtasababisha watu hawa wote waangamizwe.”

16 Baadaye wakaja tena kwake na kumwambia: “Turuhusu tujenge hapa mazizi ya mawe kwa ajili ya mifugo yetu na majiji kwa ajili ya watoto wetu. 17 Lakini sisi tutaendelea kuwa tayari kwa ajili ya vita+ na tutakuwa mstari wa mbele mpaka tutakapowafikisha Waisraeli mahali pao, wakati huo watoto wetu watakaa katika majiji yenye ngome, wakiwa salama kutoka kwa wakaaji wa nchi. 18 Hatutarudi katika nyumba zetu mpaka kila Mwisraeli atakaporithi eneo lake.+ 19 Kwa maana hatutapokea urithi wowote pamoja nao katika eneo lote lililo ng’ambo ya Yordani, kwa sababu tumepokea urithi wetu upande wa mashariki wa Yordani.”+

20 Musa akawaambia: “Ikiwa mtafanya hivi: Ikiwa mtachukua silaha mbele za Yehova kwa ajili ya vita;+ 21 na ikiwa kila mmoja wenu atachukua silaha na kuvuka Yordani mbele za Yehova anapowafukuza maadui wake kutoka mbele zake+ 22 mpaka mtakaposhinda na kuichukua nchi mbele za Yehova,+ mnaweza kurudi+ nanyi hamtakuwa na hatia mbele za Yehova na Waisraeli. Ndipo Yehova atakapokubali mmiliki nchi hii.+ 23 Lakini msipofanya hivyo, mtakuwa mmemtendea dhambi Yehova. Nanyi mjue kwamba mtaadhibiwa kwa sababu ya dhambi yenu. 24 Kwa hiyo mnaweza kujenga majiji kwa ajili ya watoto wenu na mazizi kwa ajili ya mifugo yenu,+ lakini ni lazima mfanye mambo mliyoahidi.”

25 Wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakamwambia Musa hivi: “Bwana wetu, sisi watumishi wako tutafanya kama unavyotuamuru. 26 Watoto wetu, wake zetu, mifugo yetu, na wanyama wetu wote watabaki hapa katika majiji ya Gileadi,+ 27 lakini sisi watumishi wako tutavuka, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova,+ kama unavyosema bwana wetu.”

28 Basi Musa akampa kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo* za makabila ya Waisraeli amri kuwahusu. 29 Musa akawaambia hivi: “Ikiwa wana wa Gadi na wana wa Rubeni watavuka Yordani pamoja nanyi, yaani, kila mwanamume aliyechukua silaha ili kupigana vita mbele za Yehova, nanyi mshinde na kuchukua eneo hilo, basi mtawapa eneo la Gileadi ili walimiliki.+ 30 Lakini ikiwa hawatachukua silaha na kuvuka pamoja nanyi, basi wataishi pamoja nanyi katika nchi ya Kanaani.”

31 Basi wana wa Gadi na wana wa Rubeni wakajibu: “Sisi watumishi wako tutafanya mambo ambayo Yehova ametuambia. 32 Tutachukua silaha na kuvuka mbele za Yehova kuingia nchi ya Kanaani,+ lakini urithi wetu utakuwa upande huu wa Yordani.” 33 Hivyo Musa akawapa—wana wa Gadi, wana wa Rubeni,+ na nusu ya kabila la Manase+ mwana wa Yosefu—ufalme wa Sihoni+ mfalme wa Waamori na ufalme wa Ogu+ mfalme wa Bashani, maeneo hayo na majiji yaliyokuwemo na pia majiji jirani.

34 Wana wa Gadi wakajenga* Diboni,+ Atarothi,+ Aroeri,+ 35 Atroth-shofani, Yazeri,+ Yogbeha,+ 36 Beth-nimra,+ Beth-harani,+ majiji yenye ngome, na mazizi ya mawe kwa ajili ya mifugo. 37 Nao wana wa Rubeni wakajenga Heshboni,+ Eleale,+ Kiriathaimu,+ 38 Nebo,+ na Baal-meoni+—majina ya majiji hayo yalibadilishwa—na Sibma; nao wakaanza kuyapa majina mapya majiji waliyojenga upya.

39 Wana wa Makiri+ mwana wa Manase walishambulia eneo la Gileadi, wakaliteka, na kuwafukuza Waamori waliokaa humo. 40 Kwa hiyo Musa akampa Makiri mwana wa Manase, Gileadi, akaanza kukaa katika eneo hilo.+ 41 Na Yairi mwana wa Manase akawashambulia wakaaji wa eneo hilo na kuteka vijiji vyao vya mahema, akaviita Hawoth-yairi.*+ 42 Naye Noba akashambulia na kuliteka jiji la Kenathi na miji yake, naye akaliita Noba, jina lake mwenyewe.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki