Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 42
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Kumsifu Mungu akiwa Mwokozi Mtukufu

        • Kuwa na kiu kwa ajili ya Mungu kama paa aliye na kiu ya maji (1, 2)

        • “Kwa nini nimesononeka?” (5, 11)

        • “Mngojee Mungu” (5, 11)

Zaburi 42:utangulizi

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +2Nya 20:19

Zaburi 42:2

Marejeo

  • +Zb 63:1
  • +Zb 27:4; 84:2

Zaburi 42:3

Marejeo

  • +Zb 3:2; 42:10; 79:10

Zaburi 42:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

  • *

    Au “polepole.”

Marejeo

  • +Kum 16:14, 16; 2Nya 30:23, 24

Zaburi 42:5

Marejeo

  • +Zb 55:4; Mk 14:34
  • +Zb 37:7; Omb 3:24; Mik 7:7
  • +Zb 43:5

Zaburi 42:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ule mlima mdogo.”

Marejeo

  • +Zb 22:1; Yoh 12:27
  • +Yon 2:7

Zaburi 42:7

Marejeo

  • +Zb 88:7

Zaburi 42:8

Marejeo

  • +Zb 27:1

Zaburi 42:9

Marejeo

  • +Zb 13:1
  • +Zb 38:6; 43:2

Zaburi 42:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, inayoweza kusababisha mauaji.

  • *

    Au labda, “kana kwamba wanaiponda mifupa yangu.”

Marejeo

  • +Zb 3:2; 42:3; 79:10

Zaburi 42:11

Marejeo

  • +Zb 37:7
  • +Zb 42:5; 43:5

Jumla

Zab. 42:utangulizi2Nya 20:19
Zab. 42:2Zb 63:1
Zab. 42:2Zb 27:4; 84:2
Zab. 42:3Zb 3:2; 42:10; 79:10
Zab. 42:4Kum 16:14, 16; 2Nya 30:23, 24
Zab. 42:5Zb 55:4; Mk 14:34
Zab. 42:5Zb 37:7; Omb 3:24; Mik 7:7
Zab. 42:5Zb 43:5
Zab. 42:6Zb 22:1; Yoh 12:27
Zab. 42:6Yon 2:7
Zab. 42:7Zb 88:7
Zab. 42:8Zb 27:1
Zab. 42:9Zb 13:1
Zab. 42:9Zb 38:6; 43:2
Zab. 42:10Zb 3:2; 42:3; 79:10
Zab. 42:11Zb 37:7
Zab. 42:11Zb 42:5; 43:5
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 42:1-11

Zaburi

KITABU CHA PILI

(Zaburi 42-72)

Kwa kiongozi. Maskili* ya wana wa Kora.+

42 Kama paa anayetamani vijito vya maji,

Ndivyo ninavyokutamani, Ee Mungu.

 2 Nina kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu aliye hai.+

Nije lini na kuonekana mbele za Mungu?+

 3 Machozi yangu ni chakula changu usiku na mchana;

Mchana kutwa watu wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+

 4 Ninayakumbuka mambo haya, nami naimwaga nafsi* yangu,

Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na umati;

Nilikuwa nikitembea kimyakimya* mbele zao kwenda katika nyumba ya Mungu,

Kwa sauti za shangwe na shukrani,

Za umati unaofanya sherehe.+

 5 Kwa nini nimesononeka?+

Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu.+

 6 Mungu wangu, nimesononeka.+

Ndiyo sababu ninakukumbuka,+

Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,

Kutoka Mlima Mizari.*

 7 Vilindi vya maji vinaita vilindi vya maji

Kwa sauti ya maporomoko yako ya maji.

Mawimbi yako makubwa yamenilemea.+

 8 Wakati wa mchana Yehova atanipa upendo wake mshikamanifu,

Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja nami—sala kwa Mungu wa uhai wangu.+

 9 Nitamwambia Mungu, jabali langu:

“Kwa nini umenisahau?+

Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+

10 Maadui wangu wananidhihaki kwa chuki kali sana;**

Mchana kutwa wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+

11 Kwa nini nimesononeka?

Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu?

Mngojee Mungu,+

Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu na Mungu wangu.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki