Isaya
46 Beli anainama chini,+ Nebo anainama.
Sanamu zao zimewekwa juu ya wanyama, juu ya wanyama wanaobeba mizigo,+
Kama mizigo inayowalemea wanyama waliochoka.
3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+
Ninyi niliowategemeza tangu mlipozaliwa na kuwabeba tangu tumboni.+
4 Hata utakapozeeka nitakuwa yuleyule;+
Hata kichwa chako kikiwa na mvi nitaendelea kukubeba.
Kama nilivyofanya, nitakubeba na kukuchukua na kukuokoa.+
5 Mtanifananisha na nani au kunifanya niwe sawa na nani au kunilinganisha na nani,+
Ili tufanane naye?+
6 Kuna wale wanaomwaga dhahabu kwa wingi kutoka kwenye mikoba yao;
Wanapima fedha katika mizani.
Wanamwajiri mfua chuma, naye huitengeneza kuwa mungu.+
Kisha wanasujudu, naam, wanaiabudu.*+
7 Wanaiinua na kujitwika mabegani;+
Wanaibeba na kuiweka mahali pake, nayo husimama papo hapo.
Haiondoki mahali pake.+
Wanaipazia sauti, lakini haiwajibu;
Haiwezi kumwokoa yeyote kutoka katika taabu yake.+
8 Kumbukeni hilo, na mjipe ujasiri.
Litieni moyoni, ninyi wakosaji.
9 Kumbukeni mambo ya kwanza* ya zamani za kale,
Kwamba mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.
Mimi ni Mungu, na hakuna aliye kama mimi.+
10 Tangu mwanzo ninatabiri matokeo,
Na tangu zamani za kale mambo ambayo bado hayajafanywa.+
Nimesema, nami nitalitimiza.
Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+
12 Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mkaidi,*
Ninyi mlio mbali sana na uadilifu.
Nitaleta wokovu katika Sayuni, na fahari yangu kwa Israeli.”+