Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 46
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Isaya—Yaliyomo

      • Sanamu za Babiloni dhidi ya Mungu wa Israeli (1-13)

        • Yehova atabiri mambo ya wakati ujao (10)

        • Ndege anayewinda anayetoka mashariki (11)

Isaya 46:1

Marejeo

  • +Yer 50:2; 51:44
  • +Isa 45:20

Isaya 46:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, sanamu zilizobebwa na wanyama.

Isaya 46:3

Marejeo

  • +Isa 1:9
  • +Kut 19:4; Kum 1:31; Isa 44:2

Isaya 46:4

Marejeo

  • +Isa 41:4
  • +Isa 43:13

Isaya 46:5

Marejeo

  • +Kut 15:11
  • +Mdo 17:29

Isaya 46:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wanaiinamia.”

Marejeo

  • +Isa 40:19; Yer 10:8, 9
  • +Isa 44:16, 17; Da 3:1, 5

Isaya 46:7

Marejeo

  • +Yer 10:5
  • +1Sa 5:3
  • +1Fa 18:26; Isa 37:37, 38; Yon 1:5

Isaya 46:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “awali.”

Marejeo

  • +Kum 33:26

Isaya 46:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kusudi; shauri.”

Marejeo

  • +Isa 42:9; 45:21
  • +Zb 33:11
  • +Zb 135:6; Isa 55:10, 11

Isaya 46:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “upande wa mapambazuko ya jua.”

  • *

    Au “kusudi; shauri.”

Marejeo

  • +Isa 41:2; 45:1
  • +Ezr 1:1, 2; Isa 44:28; 48:14
  • +Hes 23:19; Ayu 23:13

Isaya 46:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “moyo wenye nguvu.”

Isaya 46:13

Marejeo

  • +Isa 12:2; 51:5; 62:11
  • +Isa 44:23; 60:21

Jumla

Isa. 46:1Yer 50:2; 51:44
Isa. 46:1Isa 45:20
Isa. 46:3Isa 1:9
Isa. 46:3Kut 19:4; Kum 1:31; Isa 44:2
Isa. 46:4Isa 41:4
Isa. 46:4Isa 43:13
Isa. 46:5Kut 15:11
Isa. 46:5Mdo 17:29
Isa. 46:6Isa 40:19; Yer 10:8, 9
Isa. 46:6Isa 44:16, 17; Da 3:1, 5
Isa. 46:7Yer 10:5
Isa. 46:71Sa 5:3
Isa. 46:71Fa 18:26; Isa 37:37, 38; Yon 1:5
Isa. 46:9Kum 33:26
Isa. 46:10Isa 42:9; 45:21
Isa. 46:10Zb 33:11
Isa. 46:10Zb 135:6; Isa 55:10, 11
Isa. 46:11Isa 41:2; 45:1
Isa. 46:11Ezr 1:1, 2; Isa 44:28; 48:14
Isa. 46:11Hes 23:19; Ayu 23:13
Isa. 46:13Isa 12:2; 51:5; 62:11
Isa. 46:13Isa 44:23; 60:21
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Isaya 46:1-13

Isaya

46 Beli anainama chini,+ Nebo anainama.

Sanamu zao zimewekwa juu ya wanyama, juu ya wanyama wanaobeba mizigo,+

Kama mizigo inayowalemea wanyama waliochoka.

 2 Wanainama na kujiinamisha pamoja;

Hawawezi kuiokoa mizigo,*

Nao wenyewe wanaenda utekwani.

 3 “Nisikilize mimi, Ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote mnaobaki wa nyumba ya Israeli,+

Ninyi niliowategemeza tangu mlipozaliwa na kuwabeba tangu tumboni.+

 4 Hata utakapozeeka nitakuwa yuleyule;+

Hata kichwa chako kikiwa na mvi nitaendelea kukubeba.

Kama nilivyofanya, nitakubeba na kukuchukua na kukuokoa.+

 5 Mtanifananisha na nani au kunifanya niwe sawa na nani au kunilinganisha na nani,+

Ili tufanane naye?+

 6 Kuna wale wanaomwaga dhahabu kwa wingi kutoka kwenye mikoba yao;

Wanapima fedha katika mizani.

Wanamwajiri mfua chuma, naye huitengeneza kuwa mungu.+

Kisha wanasujudu, naam, wanaiabudu.*+

 7 Wanaiinua na kujitwika mabegani;+

Wanaibeba na kuiweka mahali pake, nayo husimama papo hapo.

Haiondoki mahali pake.+

Wanaipazia sauti, lakini haiwajibu;

Haiwezi kumwokoa yeyote kutoka katika taabu yake.+

 8 Kumbukeni hilo, na mjipe ujasiri.

Litieni moyoni, ninyi wakosaji.

 9 Kumbukeni mambo ya kwanza* ya zamani za kale,

Kwamba mimi ni Mungu, na hakuna mwingine.

Mimi ni Mungu, na hakuna aliye kama mimi.+

10 Tangu mwanzo ninatabiri matokeo,

Na tangu zamani za kale mambo ambayo bado hayajafanywa.+

Ninasema, ‘Uamuzi* wangu utasimama,+

Nami nitafanya jambo lolote ninalopenda.’+

11 Ninamwita kutoka mashariki* ndege anayewinda,+

Kutoka nchi ya mbali mtu atakayetekeleza uamuzi* wangu.+

Nimesema, nami nitalitimiza.

Nimekusudia, nami pia nitalitekeleza.+

12 Nisikilizeni, ninyi mlio na moyo mkaidi,*

Ninyi mlio mbali sana na uadilifu.

13 Nimeuleta karibu uadilifu wangu;

Hauko mbali sana,

Na wokovu wangu hautakawia.+

Nitaleta wokovu katika Sayuni, na fahari yangu kwa Israeli.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki