Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 30
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kutoka—Yaliyomo

      • Madhabahu ya uvumba (1-10)

      • Kuhesabiwa kwa watu na pesa za dhabihu ya kufunika dhambi (11-16)

      • Beseni la shaba la kunawia mikono na miguu (17-21)

      • Mchanganyiko wa pekee wa mafuta yanayotumiwa kutia mafuta (22-33)

      • Utaratibu wa kutengeneza uvumba mtakatifu (34-38)

Kutoka 30:1

Marejeo

  • +Kut 40:5
  • +Kut 37:25-28

Kutoka 30:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Kut 27:1, 2; Law 4:7

Kutoka 30:6

Marejeo

  • +Kut 26:33; Ebr 9:3
  • +Kut 25:22

Kutoka 30:7

Marejeo

  • +1Nya 23:13
  • +Kut 30:34, 35
  • +Hes 16:39, 40; 1Sa 2:27, 28; Lu 1:9
  • +Kut 27:20

Kutoka 30:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Katikati ya zile jioni mbili.”

Kutoka 30:9

Marejeo

  • +Law 10:1; 2Nya 26:18; Eze 8:11, 12

Kutoka 30:10

Marejeo

  • +Law 23:27; Ebr 9:7
  • +Law 16:5, 6, 18, 19

Kutoka 30:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uhai wake.”

Marejeo

  • +Kut 38:25; Hes 1:2; 2Sa 24:10, 15

Kutoka 30:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Au “shekeli takatifu.”

  • *

    Gera moja ilikuwa na uzito wa gramu 0.57. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Law 27:25
  • +2Nya 24:9; Mt 17:24

Kutoka 30:14

Marejeo

  • +Kut 38:26; Hes 1:3; 26:1, 2

Kutoka 30:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Tnn., “kwa ajili ya uhai wenu.”

Kutoka 30:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “uhai wenu.”

Kutoka 30:18

Marejeo

  • +Kut 38:8; Law 8:11; 1Fa 7:38
  • +Kut 40:7

Kutoka 30:19

Marejeo

  • +Kut 40:30, 31; Ebr 10:22

Kutoka 30:21

Marejeo

  • +2Nya 4:6

Kutoka 30:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “shekeli takatifu.”

  • *

    Hini ilikuwa sawa na lita 3.67. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Hes 3:47

Kutoka 30:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kama anavyofanya mtengenezaji wa manukato.”

Marejeo

  • +Kut 37:29

Kutoka 30:26

Marejeo

  • +Kut 40:9; Hes 7:1

Kutoka 30:29

Marejeo

  • +Law 8:10
  • +Kut 29:37

Kutoka 30:30

Marejeo

  • +Law 8:12
  • +Hes 3:2, 3
  • +Kut 40:15

Kutoka 30:31

Marejeo

  • +Kut 37:29; 1Fa 1:39; Zb 89:20

Kutoka 30:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mgeni,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.

Marejeo

  • +Kut 30:37, 38

Kutoka 30:34

Marejeo

  • +Kut 25:3, 6

Kutoka 30:35

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kama anavyofanya mtengenezaji wa manukato.”

Marejeo

  • +Kut 37:29; Zb 141:2; Ufu 5:8
  • +Law 2:13

Kutoka 30:37

Marejeo

  • +Kut 30:31, 32

Jumla

Kut. 30:1Kut 40:5
Kut. 30:1Kut 37:25-28
Kut. 30:2Kut 27:1, 2; Law 4:7
Kut. 30:6Kut 26:33; Ebr 9:3
Kut. 30:6Kut 25:22
Kut. 30:71Nya 23:13
Kut. 30:7Kut 30:34, 35
Kut. 30:7Hes 16:39, 40; 1Sa 2:27, 28; Lu 1:9
Kut. 30:7Kut 27:20
Kut. 30:9Law 10:1; 2Nya 26:18; Eze 8:11, 12
Kut. 30:10Law 23:27; Ebr 9:7
Kut. 30:10Law 16:5, 6, 18, 19
Kut. 30:12Kut 38:25; Hes 1:2; 2Sa 24:10, 15
Kut. 30:13Law 27:25
Kut. 30:132Nya 24:9; Mt 17:24
Kut. 30:14Kut 38:26; Hes 1:3; 26:1, 2
Kut. 30:18Kut 38:8; Law 8:11; 1Fa 7:38
Kut. 30:18Kut 40:7
Kut. 30:19Kut 40:30, 31; Ebr 10:22
Kut. 30:212Nya 4:6
Kut. 30:24Hes 3:47
Kut. 30:25Kut 37:29
Kut. 30:26Kut 40:9; Hes 7:1
Kut. 30:29Law 8:10
Kut. 30:29Kut 29:37
Kut. 30:30Law 8:12
Kut. 30:30Hes 3:2, 3
Kut. 30:30Kut 40:15
Kut. 30:31Kut 37:29; 1Fa 1:39; Zb 89:20
Kut. 30:33Kut 30:37, 38
Kut. 30:34Kut 25:3, 6
Kut. 30:35Kut 37:29; Zb 141:2; Ufu 5:8
Kut. 30:35Law 2:13
Kut. 30:37Kut 30:31, 32
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Kutoka 30:1-38

Kutoka

30 “Utajenga madhabahu ya kufukizia uvumba;+ utaijenga kwa mbao za mshita.+ 2 Itakuwa ya mraba; urefu wa mkono mmoja,* upana wa mkono mmoja, na kimo cha mikono miwili. Pembe zake zitakuwa sehemu ya madhabahu hiyo.+ 3 Utaifunika kwa dhahabu safi: sehemu yake ya juu, pande zote kuizunguka, na pembe zake; nawe utatengeneza ukingo wa dhahabu kuizunguka. 4 Pia, utaitengenezea pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, na pete hizo zitashikilia fito za kubebea madhabahu. 5 Tengeneza fito za mshita na kuzifunika kwa dhahabu. 6 Utaiweka mbele ya pazia lililo karibu na sanduku la Ushahidi,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya sanduku la Ushahidi, mahali nitakapokutokea.+

7 “Haruni+ atafukiza uvumba wenye manukato+ juu ya madhabahu hiyo+ kila asubuhi anaposhughulikia taa.+ 8 Pia, Haruni anapowasha taa jioni kabla ya giza kuingia,* atafukiza uvumba. Ni uvumba unaofukizwa kwa ukawaida mbele za Yehova katika vizazi vyenu vyote. 9 Hampaswi kufukiza uvumba usio halali+ au kutoa juu yake dhabihu ya kuteketezwa au toleo la nafaka, wala hampaswi kumimina juu yake toleo la kinywaji. 10 Haruni anapaswa kutoa dhabihu ya kufunika dhambi juu ya pembe za madhabahu hiyo mara moja kwa mwaka.+ Akitumia kiasi fulani cha damu ya dhabihu ya dhambi inayotolewa ili kufunika dhambi,+ ataitakasa mara moja kwa mwaka katika vizazi vyenu vyote. Ni madhabahu takatifu zaidi kwa Yehova.”

11 Kisha Yehova akamwambia Musa: 12 “Wakati wowote unapowahesabu wana wa Israeli,+ ni lazima kila mmoja wao anipe mimi Yehova fidia kwa ajili ya nafsi yake* watu wanapohesabiwa. Watafanya hivyo ili wasipatwe na pigo lolote wanapoandikishwa. 13 Wote watakaoandikishwa watatoa nusu ya shekeli* kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ Gera 20* ni sawa na shekeli moja. Nusu shekeli ni mchango kwa Yehova.+ 14 Kila mtu mwenye umri wa kuanzia miaka 20 anayeandikishwa atatoa mchango wa Yehova.+ 15 Tajiri hapaswi kutoa zaidi na maskini hapaswi kutoa mchango wa Yehova unaopungua nusu shekeli* ili kutoa dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya nafsi zenu.* 16 Unapaswa kuchukua kutoka kwa Waisraeli fedha za dhabihu ya kufunika dhambi na kuzitoa ili zitumiwe katika utumishi wa hema la mkutano, ziwe kumbukumbu mbele za Yehova kwa ajili ya Waisraeli, ili kufunika dhambi kwa ajili ya nafsi zenu.”*

17 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 18 “Tengeneza beseni la kunawia la shaba pamoja na kinara chake;+ kisha uliweke kati ya hema la mkutano na madhabahu na utie maji ndani yake.+ 19 Haruni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwenye beseni hilo.+ 20 Wanapoingia kwenye hema la mkutano au wanapoenda kwenye madhabahu kuhudumu na kumtolea Yehova dhabihu za kuteketezwa na zinazofuka moshi, watanawa kwa maji ili wasife. 21 Ni lazima wanawe mikono na miguu ili wasife, nayo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yao, yaani, kwa Haruni na uzao wake, katika vizazi vyao vyote.”+

22 Yehova akaendelea kumwambia Musa: 23 “Kisha, chukua manukato bora kabisa: kilogramu 6 za manemane iliyoganda, kilogramu 3 za mdalasini wenye harufu nzuri, kilogramu 3 za kane, 24 na kilogramu 6 za kida, zilizopimwa kwa shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,*+ pamoja na hini moja* ya mafuta ya zeituni. 25 Kisha utumie manukato hayo kutengeneza mafuta matakatifu ya kutia mafuta; manukato hayo yanapaswa kuchanganywa pamoja kwa ustadi.*+ Yatakuwa mafuta matakatifu ya kutia mafuta.

26 “Utayatumia kutia mafuta hema la mkutano+ na sanduku la Ushahidi, 27 pamoja na meza na vyombo vyake vyote, kinara cha taa na vyombo vyake, madhabahu ya uvumba, 28 madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na lile beseni pamoja na kinara chake. 29 Ni lazima uvitakase ili viwe vitakatifu kabisa.+ Yeyote anayevigusa anapaswa kuwa mtakatifu.+ 30 Nawe utamtia mafuta Haruni+ na wanawe+ na kuwatakasa ili wanitumikie wakiwa makuhani.+

31 “Nawe utawaambia Waisraeli, ‘Mafuta haya ya kutia mafuta yataendelea kuwa matakatifu kwangu katika vizazi vyenu.+ 32 Hayapaswi kupakwa kwenye ngozi ya mwanadamu, nanyi hampaswi kutengeneza kitu chochote chenye mchanganyiko kama huo. Ni mafuta matakatifu. Yataendelea kuwa matakatifu kwenu. 33 Mtu yeyote anayetengeneza mafuta kama hayo na kumpaka mtu asiye na idhini* ni lazima auawe.’”+

34 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Chukua vipimo vinavyolingana vya manukato haya:+ matone ya natafi, shekelethi, kelbena yenye manukato, na ubani safi. 35 Yatumie kutengeneza uvumba;+ viungo hivyo vinapaswa kuchanganywa kwa ustadi,* vitiwe chumvi,+ viwe safi, na vitakatifu. 36 Utaponda baadhi ya viungo hivyo viwe unga laini na kuweka kiasi fulani mbele ya sanduku la Ushahidi katika hema la mkutano, mahali nitakapokutokea. Mchanganyiko huo unapaswa kuwa mtakatifu kabisa kwenu. 37 Hampaswi kutumia mchanganyiko huo kujitengenezea uvumba kwa ajili ya matumizi yenu.+ Mnapaswa kuuona kuwa mtakatifu kwa Yehova. 38 Yeyote atakayetengeneza uvumba kama huo ili afurahie harufu yake ni lazima auawe.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki