Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 20
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Sara aokolewa kutoka mikononi mwa Abimeleki (1-18)

Mwanzo 20:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “akiishi akiwa mgeni.”

Marejeo

  • +Mwa 13:18
  • +Hes 13:26
  • +Mwa 25:17, 18
  • +Mwa 10:19; 26:6

Mwanzo 20:2

Marejeo

  • +Mwa 12:11-13; 20:11, 12
  • +Mwa 12:15

Mwanzo 20:3

Marejeo

  • +Mwa 12:17; Zb 105:14
  • +Kum 22:22

Mwanzo 20:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, hakuwa amefanya naye ngono.

  • *

    Au “ni adilifu.”

Mwanzo 20:7

Marejeo

  • +Zb 105:14, 15
  • +Ayu 42:8

Mwanzo 20:10

Marejeo

  • +Mwa 12:18, 19; 26:9, 10

Mwanzo 20:11

Marejeo

  • +Mwa 12:11, 12; 26:7

Mwanzo 20:12

Marejeo

  • +Mwa 11:29

Mwanzo 20:13

Marejeo

  • +Mwa 12:1
  • +Mwa 12:13

Mwanzo 20:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Tazama, ni kifuniko cha macho kwako.”

Marejeo

  • +Mwa 20:2, 12

Mwanzo 20:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “alikuwa amefunga kabisa kila tumbo la uzazi la nyumba ya Abimeleki.”

Marejeo

  • +Mwa 12:17

Jumla

Mwa. 20:1Mwa 13:18
Mwa. 20:1Hes 13:26
Mwa. 20:1Mwa 25:17, 18
Mwa. 20:1Mwa 10:19; 26:6
Mwa. 20:2Mwa 12:11-13; 20:11, 12
Mwa. 20:2Mwa 12:15
Mwa. 20:3Mwa 12:17; Zb 105:14
Mwa. 20:3Kum 22:22
Mwa. 20:7Zb 105:14, 15
Mwa. 20:7Ayu 42:8
Mwa. 20:10Mwa 12:18, 19; 26:9, 10
Mwa. 20:11Mwa 12:11, 12; 26:7
Mwa. 20:12Mwa 11:29
Mwa. 20:13Mwa 12:1
Mwa. 20:13Mwa 12:13
Mwa. 20:16Mwa 20:2, 12
Mwa. 20:18Mwa 12:17
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 20:1-18

Mwanzo

20 Sasa Abrahamu akaihamisha kambi yake kutoka huko+ na kwenda katika nchi ya Negebu, akaanza kuishi kati ya Kadeshi+ na Shuri.+ Alipokuwa akiishi* Gerari,+ 2 Abrahamu akasema tena kumhusu Sara mke wake: “Huyu ni dada yangu.”+ Kwa hiyo Abimeleki mfalme wa Gerari akaagiza Sara aletwe, naye akamchukua.+ 3 Baadaye, Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto usiku na kumwambia: “Wewe ni kama mtu aliyekufa kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemchukua,+ kwa maana ameolewa naye ni mke wa mwanamume mwingine.”+ 4 Hata hivyo, Abimeleki hakuwa amemkaribia.* Kwa hiyo akasema: “Yehova, je, utaliua taifa ambalo kwa kweli halina hatia?* 5 Je, yeye hakuniambia, ‘Huyu ni dada yangu,’ na mwanamke huyu pia hakuniambia, ‘Huyu ni ndugu yangu’? Nilifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu na mikono isiyo na hatia.” 6 Kisha Mungu wa kweli akamwambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee dhambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umguse. 7 Sasa mrudishe mke wa mwanamume huyo, kwa maana mwanamume huyo ni nabii,+ atakuombea dua,+ nawe utaendelea kuishi. Lakini usipomrudisha, ujue kwamba kwa hakika utakufa, wewe na watu wako wote.”

8 Abimeleki akaamka asubuhi na mapema akawaita watumishi wake wote na kuwaambia mambo hayo yote, nao wakaogopa sana. 9 Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia: “Ni jambo gani hili ulilotutendea? Nimekutendea dhambi gani hivi kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi kubwa hivi? Jambo ulilonitendea si sawa.” 10 Na Abimeleki akaendelea kumwambia Abrahamu: “Ulikuwa na nia gani ulipofanya jambo hili?”+ 11 Abrahamu akasema: “Ni kwa sababu nilisema moyoni mwangu, ‘Hakika watu wa mahali hapa hawamwogopi Mungu, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’+ 12 Na isitoshe, kwa kweli huyu ni dada yangu, binti ya baba yangu lakini si binti ya mama yangu, naye akawa mke wangu.+ 13 Kwa hiyo Mungu aliponifanya nitangetange kutoka katika nyumba ya baba yangu,+ nilimwambia mke wangu: ‘Hivi ndivyo utakavyonionyesha upendo mshikamanifu: Kila mahali tutakapokwenda, sema hivi kunihusu, “Huyu ni ndugu yangu.”’”+

14 Basi Abimeleki akachukua kondoo na ng’ombe na watumishi wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, naye akamrudishia Abrahamu mke wake, Sara. 15 Pia Abimeleki akasema: “Tazama nchi yangu iko wazi mbele yako. Ishi popote unapopenda.” 16 Naye akamwambia Sara: “Tazama ninampa ndugu yako vipande 1,000 vya fedha.+ Ni ishara ya kwamba huna hatia* mbele ya wote walio pamoja nawe na mbele ya watu wote, nawe umeondolewa shutuma.” 17 Na Abrahamu akaanza kumwomba dua Mungu wa kweli, naye Mungu akamponya Abimeleki na mke wake na vijakazi wake, nao wakaanza kuzaa watoto; 18 kwa maana Yehova alikuwa amewafanya wanawake wote wa nyumba ya Abimeleki wawe tasa* kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.+

Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki