Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 4
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Matendo—Yaliyomo

      • Petro na Yohana wakamatwa (1-4)

        • Idadi ya waamini yafikia wanaume 5,000 (4)

      • Kesi mbele ya Sanhedrini (5-22)

        • “Hatuwezi kuacha kusema” (20)

      • Wasali ili wapate ujasiri (23-31)

      • Wanafunzi washiriki vitu vyao pamoja (32-37)

Matendo 4:1

Marejeo

  • +Mdo 23:8

Matendo 4:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kufufuliwa kutoka kwa wafu katika kisa cha Yesu.”

Marejeo

  • +Mdo 4:33; 17:18

Matendo 4:3

Marejeo

  • +Lu 21:12

Matendo 4:4

Marejeo

  • +Mdo 2:41; 6:7

Matendo 4:6

Marejeo

  • +Yoh 18:13
  • +Mt 26:57; Lu 3:2; Yoh 11:49-51

Matendo 4:8

Marejeo

  • +Mdo 7:55

Matendo 4:9

Marejeo

  • +Mdo 3:7

Matendo 4:10

Marejeo

  • +Mdo 3:6
  • +Mdo 2:36
  • +Mdo 2:24; 5:30

Matendo 4:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kichwa cha pembeni.”

Marejeo

  • +Zb 118:22; Isa 28:16; Mt 21:42; 1Pe 2:7

Matendo 4:12

Marejeo

  • +Mt 1:21; Mdo 10:43; Flp 2:9, 10
  • +Yoh 1:12; 14:6; 1Ti 2:5, 6

Matendo 4:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, hawakuwa na elimu ya shule za kirabi; haimaanishi hawakujua kusoma na kuandika.

Marejeo

  • +Mt 11:25; 1Ko 1:26, 27
  • +Yoh 7:14, 15

Matendo 4:14

Marejeo

  • +Mdo 3:11
  • +Lu 21:15

Matendo 4:16

Marejeo

  • +Yoh 11:47
  • +Mdo 3:9, 10

Matendo 4:17

Marejeo

  • +Mdo 5:40

Matendo 4:20

Marejeo

  • +Mdo 5:29

Matendo 4:21

Marejeo

  • +Lu 22:2; Mdo 5:26

Matendo 4:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ishara hiyo.”

Matendo 4:24

Marejeo

  • +Kut 20:11; Ne 9:6; Zb 146:6

Matendo 4:25

Marejeo

  • +2Sa 23:1, 2

Matendo 4:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

  • *

    Au “Kristo wake.”

Marejeo

  • +Zb 2:1, 2

Matendo 4:27

Marejeo

  • +Lu 23:12
  • +Zb 45:7; Mdo 10:38

Matendo 4:28

Marejeo

  • +Isa 53:10; Lu 24:44; Mdo 2:23; 1Pe 1:20

Matendo 4:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Matendo 4:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “miujiza.”

Marejeo

  • +Mdo 2:43; 5:12
  • +Mdo 3:16

Matendo 4:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “waliposali kwa bidii.”

Marejeo

  • +Mdo 2:2, 4
  • +1Th 2:2

Matendo 4:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Mdo 2:44, 45

Matendo 4:33

Marejeo

  • +Mdo 1:21, 22; 4:2

Matendo 4:34

Marejeo

  • +Mdo 2:44, 45

Matendo 4:35

Marejeo

  • +Mdo 5:1, 2
  • +Mdo 6:1

Matendo 4:36

Marejeo

  • +Mdo 11:22; 12:25

Matendo 4:37

Marejeo

  • +Lu 12:33

Jumla

Mdo. 4:1Mdo 23:8
Mdo. 4:2Mdo 4:33; 17:18
Mdo. 4:3Lu 21:12
Mdo. 4:4Mdo 2:41; 6:7
Mdo. 4:6Yoh 18:13
Mdo. 4:6Mt 26:57; Lu 3:2; Yoh 11:49-51
Mdo. 4:8Mdo 7:55
Mdo. 4:9Mdo 3:7
Mdo. 4:10Mdo 3:6
Mdo. 4:10Mdo 2:36
Mdo. 4:10Mdo 2:24; 5:30
Mdo. 4:11Zb 118:22; Isa 28:16; Mt 21:42; 1Pe 2:7
Mdo. 4:12Mt 1:21; Mdo 10:43; Flp 2:9, 10
Mdo. 4:12Yoh 1:12; 14:6; 1Ti 2:5, 6
Mdo. 4:13Mt 11:25; 1Ko 1:26, 27
Mdo. 4:13Yoh 7:14, 15
Mdo. 4:14Mdo 3:11
Mdo. 4:14Lu 21:15
Mdo. 4:16Yoh 11:47
Mdo. 4:16Mdo 3:9, 10
Mdo. 4:17Mdo 5:40
Mdo. 4:20Mdo 5:29
Mdo. 4:21Lu 22:2; Mdo 5:26
Mdo. 4:24Kut 20:11; Ne 9:6; Zb 146:6
Mdo. 4:252Sa 23:1, 2
Mdo. 4:26Zb 2:1, 2
Mdo. 4:27Lu 23:12
Mdo. 4:27Zb 45:7; Mdo 10:38
Mdo. 4:28Isa 53:10; Lu 24:44; Mdo 2:23; 1Pe 1:20
Mdo. 4:30Mdo 2:43; 5:12
Mdo. 4:30Mdo 3:16
Mdo. 4:31Mdo 2:2, 4
Mdo. 4:311Th 2:2
Mdo. 4:32Mdo 2:44, 45
Mdo. 4:33Mdo 1:21, 22; 4:2
Mdo. 4:34Mdo 2:44, 45
Mdo. 4:35Mdo 5:1, 2
Mdo. 4:35Mdo 6:1
Mdo. 4:36Mdo 11:22; 12:25
Mdo. 4:37Lu 12:33
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Matendo 4:1-37

Matendo ya Mitume

4 Hao wawili walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani, kapteni wa hekalu, na Masadukayo+ wakawajia. 2 Walikuwa wameudhika kwa sababu mitume walikuwa wakiwafundisha watu na kutangaza waziwazi kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu.*+ 3 Basi wakawakamata na kuwaweka kizuizini+ mpaka siku iliyofuata, kwa maana tayari ilikuwa jioni. 4 Hata hivyo, wengi waliokuwa wamesikiliza maneno hayo wakaamini, na idadi ya wanaume ikawa karibu 5,000.+

5 Siku iliyofuata watawala wao, wazee, na waandishi wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu 6 pamoja na Anasi+ mkuu wa makuhani, Kayafa,+ Yohana, Aleksanda, na wote waliokuwa watu wa ukoo wa mkuu wa makuhani. 7 Wakawasimamisha Petro na Yohana katikati yao na kuanza kuwauliza: “Mlifanya jambo hilo kwa nguvu gani au katika jina la nani?” 8 Ndipo Petro, akiwa amejaa roho takatifu,+ akawaambia:

“Watawala wa watu na wazee, 9 ikiwa tunahojiwa leo kuhusu tendo jema alilofanyiwa mtu huyu aliyekuwa kilema,+ na ikiwa mnataka kujua aliyemponya, 10 na ijulikane kwenu nyote na kwa watu wote wa Israeli kwamba katika jina la Yesu Kristo Mnazareti,+ ambaye mlimuua kwenye mti+ lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu,+ kupitia kwake mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa ameponywa. 11 Hilo ndilo ‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilitendea kana kwamba halina maana nalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’*+ 12 Zaidi ya hayo, hakuna wokovu katika mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine+ chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo tunaweza kuokolewa.”+

13 Walipoona Petro na Yohana wakizungumza kwa ujasiri, ingawa walikuwa watu wasio na elimu* na wa kawaida tu,+ wakashangaa. Nao wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.+ 14 Walipokuwa wakimtazama yule mtu aliyekuwa ameponywa, akiwa amesimama pamoja nao,+ hawakuwa na jambo la kusema.+ 15 Basi wakawaamuru waende nje ya jumba la Sanhedrini, kisha wakaanza kushauriana, 16 wakisema: “Tufanye nini na watu hawa?+ Kwa sababu kwa kweli ishara kubwa imetukia kupitia kwao ambayo imejulikana na wakaaji wote wa Yerusalemu,+ nasi hatuwezi kuikana. 17 Ili jambo hili lisizidi kusambazwa kati ya watu, basi tuwatishe na kuwaambia wasizungumze tena na mtu yeyote kwa msingi wa jina hilo.”+

18 Ndipo wakawaita na kuwaamuru wasiseme lolote wala kufundisha kwa msingi wa jina la Yesu. 19 Lakini Petro na Yohana wakawajibu: “Kama ni sawa machoni pa Mungu kuwasikiliza ninyi badala ya Mungu, hukumuni ninyi wenyewe. 20 Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema kuhusu mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”+ 21 Basi baada ya kuwatisha zaidi, wakawafungua, kwa vile hawakupata msingi wowote wa kuwaadhibu na kwa kuwa waliwaogopa watu,+ kwani wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa sababu ya jambo lililokuwa limetukia. 22 Kwa maana yule mtu ambaye alifanyiwa muujiza huo* wa kuponywa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 40.

23 Baada ya kufunguliwa, wakaenda kwa watu wao na kuwaeleza mambo waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee. 24 Waliposikia hayo, wote kwa pamoja wakasali kwa Mungu wakisema kwa sauti kubwa:

“Bwana Mwenye Enzi Kuu, wewe Ndiye uliyeumba mbingu, dunia, bahari, na vitu vyote vilivyomo,+ 25 nawe ulisema kupitia roho takatifu kwa kinywa cha babu yetu Daudi,+ mtumishi wako: ‘Kwa nini mataifa yalikuwa na msukosuko na watu wakatafakari mambo matupu? 26 Wafalme wa dunia walijipanga nao watawala wakakusanyika pamoja kama kitu kimoja dhidi ya Yehova* na dhidi ya mtiwa-mafuta wake.’*+ 27 Kwa kweli Herode na Pontio Pilato+ pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli walikusanyika katika jiji hili dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimtia mafuta,+ 28 ili wafanye yale ambayo mkono na shauri lako liliazimia awali yatukie.+ 29 Na sasa, Yehova,* angalia vitisho vyao, nawe uwawezeshe watumwa wako waendelee kutangaza neno lako kwa ujasiri wote, 30 huku ukinyoosha mkono wako ili uponye, na huku ishara na mambo ya ajabu* yakitukia+ kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”+

31 Na baada ya kutoa dua,* mahali walipokuwa wamekusanyika pakatikiswa, na kila mmoja wao akajazwa roho takatifu+ nao walikuwa wakitangaza neno la Mungu kwa ujasiri.+

32 Isitoshe, umati uliokuwa umeamini ulikuwa na moyo na nafsi* moja, na hakuna hata mmoja wao aliyeona vitu vyake kuwa mali yake mwenyewe, bali walishiriki pamoja vitu vyote walivyokuwa navyo.+ 33 Na kwa nguvu nyingi, mitume wakaendelea kutoa ushahidi kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu,+ na fadhili zisizostahiliwa zilikuwa pamoja nao kwa kadiri kubwa. 34 Kwa kweli, hakuna yeyote kati yao aliyekuwa na uhitaji,+ kwa maana wote waliokuwa na mashamba au nyumba walikuwa wakiuza na kuleta thamani ya kile walichouza, 35 na kukiweka miguuni pa mitume.+ Kisha kila mmoja aligawiwa kulingana na uhitaji wake.+ 36 Kwa hiyo Yosefu, ambaye pia mitume walimwita Barnaba+ (jina ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Mwana wa Faraja”), Mlawi, mzaliwa wa Kipro, 37 alikuwa na shamba, akaliuza, akaleta pesa na kuziweka miguuni pa mitume.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki