Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wakorintho 12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Wakorintho—Yaliyomo

      • Maono ya Paulo (1-7a)

      • “Mwiba katika mwili” wa Paulo (7b-10)

      • Hajapungukiwa kuliko mitume walio bora sana (11-13)

      • Paulo awahangaikia Wakorintho (14-21)

2 Wakorintho 12:1

Marejeo

  • +Mdo 2:17
  • +Mdo 22:17, 18

2 Wakorintho 12:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kunipiga.”

Marejeo

  • +Gal 4:13

2 Wakorintho 12:9

Marejeo

  • +Isa 40:29

2 Wakorintho 12:10

Marejeo

  • +Flp 4:13

2 Wakorintho 12:11

Marejeo

  • +2Ko 11:23

2 Wakorintho 12:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “miujiza.”

Marejeo

  • +2Ko 6:4
  • +Mdo 14:3; 15:12; Ro 15:18, 19

2 Wakorintho 12:13

Marejeo

  • +1Ko 9:11, 12; 2Ko 11:9

2 Wakorintho 12:14

Marejeo

  • +Mdo 20:33
  • +1Ko 4:14

2 Wakorintho 12:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi zenu.”

Marejeo

  • +2Ko 1:6; Kol 1:24; 1Th 2:8; Ebr 13:17

2 Wakorintho 12:16

Marejeo

  • +2Ko 11:9

2 Wakorintho 12:18

Marejeo

  • +2Ko 8:6

2 Wakorintho 12:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “umbeya.”

2 Wakorintho 12:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.

  • *

    Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.

Jumla

2 Kor. 12:1Mdo 2:17
2 Kor. 12:1Mdo 22:17, 18
2 Kor. 12:7Gal 4:13
2 Kor. 12:9Isa 40:29
2 Kor. 12:10Flp 4:13
2 Kor. 12:112Ko 11:23
2 Kor. 12:122Ko 6:4
2 Kor. 12:12Mdo 14:3; 15:12; Ro 15:18, 19
2 Kor. 12:131Ko 9:11, 12; 2Ko 11:9
2 Kor. 12:14Mdo 20:33
2 Kor. 12:141Ko 4:14
2 Kor. 12:152Ko 1:6; Kol 1:24; 1Th 2:8; Ebr 13:17
2 Kor. 12:162Ko 11:9
2 Kor. 12:182Ko 8:6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
2 Wakorintho 12:1-21

Barua ya Pili kwa Wakorintho

12 Lazima nijisifu. Hakuna faida, lakini nitaenda kwenye maono+ ya miujiza na ufunuo wa Bwana.+ 2 Ninamjua mtu fulani katika muungano na Kristo, ambaye miaka 14 iliyopita—kama ni katika mwili au nje ya mwili, sijui; Mungu anajua—alinyakuliwa mpaka kwenye mbingu ya tatu. 3 Ndiyo, ninamjua mtu kama huyo—iwe ni katika mwili au bila mwili, mimi sijui; Mungu anajua— 4 ambaye alinyakuliwa kuingia katika paradiso na kusikia maneno yasiyoweza kutamkwa na ambayo si halali kwa mtu kuyasema. 5 Nitajisifu kuhusu mtu wa namna hiyo, lakini sitajisifu kuhusu mimi mwenyewe isipokuwa kuhusu udhaifu wangu. 6 Kwa maana hata nikitaka kujisifu, sitakuwa mtu asiye na akili, kwa kuwa nitasema ukweli. Lakini sitaki kufanya hivyo, ili yeyote asinisifu zaidi ya yale anayoona kwangu au kusikia kutoka kwangu, 7 kwa sababu tu ya kupokea maono hayo ya ajabu.

Ili nisijiinue mno, nilipewa mwiba katika mwili,+ malaika wa Shetani, aendelee kunipiga kofi,* ili nisijiinue kupita kiasi. 8 Mara tatu nilimwomba Bwana kuhusu jambo hili, kwamba aniondolee. 9 Lakini akaniambia: “Fadhili zangu zisizostahiliwa zinakutosha, kwa kuwa nguvu zangu zinakamilika katika udhaifu.”+ Kwa furaha zaidi, basi, nitajisifu kuhusu udhaifu wangu, ili nguvu za Kristo zibaki juu yangu kama hema. 10 Basi ninapendezwa na udhaifu, na matusi, na nyakati za uhitaji, na mateso na shida, kwa ajili ya Kristo. Kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.+

11 Nimekuwa mtu asiye na akili. Mlinilazimisha kuwa hivyo, kwa sababu ninyi mlipaswa kunipendekeza. Kwa maana hata katika jambo moja sikuwa mdogo kuliko mitume wenu walio bora sana, hata kama mimi si kitu.+ 12 Kwa kweli, ishara za mtume zilitokezwa kati yenu kwa uvumilivu mkubwa,+ na kwa ishara na mambo ya ajabu* na matendo yenye nguvu.+ 13 Ni kwa njia gani mlikosa kupendelewa kuliko makutaniko mengine, isipokuwa kwamba mimi mwenyewe sikuwa mzigo kwenu?+ Mnisamehe kosa hili kwa fadhili.

14 Tazama! Hii ni mara ya tatu niliyo tayari kuja kwenu, nami sitakuwa mzigo. Kwa kuwa ninawatafuta ninyi, si mali zenu;+ kwa maana watoto+ hawatarajiwi kuweka akiba kwa ajili ya wazazi wao, bali wazazi kwa ajili ya watoto wao. 15 Kwa upande wangu, nitatumia kwa furaha zaidi na kutumiwa kabisa kwa ajili yenu.*+ Kama nikiwapenda ninyi sana, je, mimi nipendwe kidogo? 16 Lakini hata iweje, mimi sikuwa mzigo kwenu.+ Hata hivyo mnasema, nilikuwa “mjanja” na niliwashika “kwa ujanja.” 17 Sikujifaidi kutoka kwenu kupitia yeyote kati ya wale niliowatuma kwenu, sivyo? 18 Nilimhimiza Tito na nikamtuma yule ndugu pamoja naye. Je, kweli Tito alijifaidi kutoka kwenu?+ Tulitembea katika roho ileile, sivyo? Katika hatua zilezile, sivyo?

19 Je, mnafikiri kwamba muda huu wote tumekuwa tukijitetea kwenu? Tunazungumza mbele za Mungu katika muungano na Kristo. Lakini wapendwa, yote tunayofanya ni kwa ajili ya kuwajenga. 20 Kwa maana ninaogopa kwamba huenda nitakapofika, sitawakuta mkiwa kama ninavyotaka nami sitakuwa kama mnavyotaka, badala yake, huenda kuna mizozo, wivu, milipuko ya hasira, migawanyiko, masengenyo, minong’ono,* kujivuna kwa kiburi, na machafuko. 21 Labda nitakapokuja tena, huenda Mungu wangu akaninyenyekeza mbele yenu, nami niwaombolezee wengi kati ya wale ambao mwanzoni walitenda dhambi lakini hawajatubu unajisi wao na uasherati* na mwenendo mpotovu* ambao wametenda.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki