Methali
4 Wanangu, sikilizeni nidhamu ya baba;+
Sikilizeni kwa makini ili mpate uelewaji,
2 Kwa maana nitawapa mafundisho mema;
4 Baba alinifundisha na kusema: “Moyo wako na ushike kabisa maneno yangu.+
Shika amri zangu, uendelee kuishi.+
5 Jipatie hekima, jipatie uelewaji.+
Usisahau, wala usiache ninayosema.
6 Usiiache, nayo itakukinga.
Ipende, nayo itakulinda.
7 Hekima ndilo jambo muhimu zaidi,*+ kwa hiyo jipatie hekima,
Pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji.+
8 Ithamini sana, nayo itakukweza.+
Itakuheshimu kwa sababu unaikumbatia.+
9 Itakuvika shada lenye kuvutia kichwani;
Itakupamba kwa taji maridadi.”
10 Mwanangu, sikiliza maneno yangu na uyakubali,
Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+
12 Unapotembea, hatua zako hazitazuiwa;
Na ukikimbia, hutajikwaa.
13 Shika kabisa nidhamu; usiiache.+
Ilinde, kwa maana ni uzima wako.+
14 Usiingie katika kijia cha waovu,
Wala usitembee katika njia ya watu wabaya.+
16 Kwa maana hawawezi kulala wasipotenda uovu.
Hawapati usingizi wasipomwangusha mtu.
17 Wanajilisha mkate wa uovu,
Na kunywa divai ya ukatili.
18 Lakini kijia cha waadilifu ni kama nuru nyangavu ya asubuhi
Inayong’aa zaidi na zaidi mpaka mchana kamili.+
19 Njia ya waovu ni kama giza;
Hawajui ni nini kinachowafanya wajikwae.
20 Mwanangu, sikiliza maneno yangu;
Sikiliza kwa makini* ninayokwambia.
21 Yasiondoke machoni pako;
Yaweke ndani kabisa moyoni mwako,+
22 Kwa maana ni uzima kwa wale wanaoyapata+
Na afya kwa mwili wao wote.
23 Ulinde moyo wako kuliko vitu vyote unavyolinda,+
Kwa maana humo ndimo zinamotoka chemchemi za uzima.
24 Jiepushe kabisa na maneno yaliyopotoka,+
Na ujitenge mbali na mazungumzo yenye hila.
25 Macho yako yanapaswa kutazama mbele moja kwa moja,
27 Usielekee kulia wala kushoto.+
Iepushe miguu yako na lililo ovu.