Zaburi
Wa Daudi, alipojifanya mwenda wazimu+ mbele ya Abimeleki, hivi kwamba akamfukuza, naye akaenda zake.
א [Aleph]
34 Nitamsifu Yehova nyakati zote;
Sifa yake itakuwa midomoni mwangu daima.
ב [Beth]
ג [Gimel]
3 Mtukuzeni Yehova pamoja nami;+
Na tulikweze jina lake pamoja.
ד [Daleth]
4 Nilimwomba Yehova ushauri, naye akanijibu.+
Aliniokoa kutoka katika mambo yote yanayoniogopesha.+
ה [He]
5 Wale waliomtazama waling’aa;
Nyuso zao hazingeweza kuona aibu.
ז [Zayin]
6 Mtu huyo wa hali ya chini aliita, na Yehova akasikia.
Alimwokoa kutoka katika taabu zake zote.+
ח [Heth]
ט [Teth]
8 Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema;+
Mwenye furaha ni mtu anayemkimbilia.
י [Yod]
9 Mwogopeni Yehova, ninyi nyote watakatifu wake,
Kwa maana wale wanaomwogopa hawakosi chochote.+
כ [Kaph]
10 Hata wanasimba* wenye nguvu wamelemewa na njaa,
Lakini wale wanaomtafuta Yehova hawatakosa chochote chema.+
ל [Lamed]
11 Njooni, wanangu, nisikilizeni;
Nitawafundisha kumwogopa Yehova.+
מ [Mem]
12 Ni nani miongoni mwenu anayependa uzima
Na angependa kuishi siku nyingi njema?+
נ [Nun]
ס [Samekh]
ע [Ayin]
15 Macho ya Yehova yanawatazama waadilifu,+
Na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba msaada.+
פ [Pe]
16 Lakini uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda maovu,
Ili afutilie mbali kumbukumbu lao lote kutoka duniani.+
צ [Tsade]
ק [Qoph]
ר [Resh]
ש [Shin]
20 Anailinda mifupa yake yote;
Haujavunjwa hata mmoja.+
ת [Taw]
21 Msiba utamuua mwovu;
Wale wanaomchukia mwadilifu watahesabiwa kuwa na hatia.