Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufunuo 13
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ufunuo—Yaliyomo

      • Mnyama-mwitu mwenye vichwa saba atoka baharini (1-10)

      • Mnyama-mwitu mwenye pembe mbili atoka duniani (11-13)

      • Sanamu ya mnyama-mwitu mwenye vichwa saba (14, 15)

      • Alama na namba ya mnyama-mwitu (16-18)

Ufunuo 13:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, yule joka.

  • *

    Au “tepe kumi za kichwani za kifalme.”

Marejeo

  • +Ufu 11:7; 13:18
  • +Isa 57:20; Ufu 21:1

Ufunuo 13:2

Marejeo

  • +Ufu 12:9
  • +Lu 4:6

Ufunuo 13:3

Marejeo

  • +Ufu 13:14

Ufunuo 13:5

Marejeo

  • +Ufu 11:2, 3

Ufunuo 13:6

Marejeo

  • +Da 7:25
  • +Ufu 12:12

Ufunuo 13:7

Marejeo

  • +Ufu 12:17

Ufunuo 13:8

Marejeo

  • +Ufu 3:5; 21:27
  • +Isa 53:7; Mt 27:50; Ufu 5:6, 12

Ufunuo 13:9

Marejeo

  • +Mt 11:15

Ufunuo 13:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Ikiwa yeyote atalazimika kuuawa.”

Marejeo

  • +Mt 26:52
  • +Da 7:18; 1Ko 6:2; Ufu 20:6
  • +Mt 24:13; Ebr 10:36; 12:3
  • +Ufu 2:10

Ufunuo 13:11

Marejeo

  • +Ufu 16:13; 20:2

Ufunuo 13:12

Marejeo

  • +Ufu 13:1
  • +Ufu 13:3

Ufunuo 13:14

Marejeo

  • +Ufu 19:20; 20:4
  • +Ufu 13:3

Ufunuo 13:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “roho.”

Ufunuo 13:16

Marejeo

  • +Ufu 14:9, 10; 16:2; 19:20

Ufunuo 13:17

Marejeo

  • +Ufu 14:11
  • +Ufu 15:2

Ufunuo 13:18

Marejeo

  • +Da 3:1

Jumla

Ufu. 13:1Ufu 11:7; 13:18
Ufu. 13:1Isa 57:20; Ufu 21:1
Ufu. 13:2Ufu 12:9
Ufu. 13:2Lu 4:6
Ufu. 13:3Ufu 13:14
Ufu. 13:5Ufu 11:2, 3
Ufu. 13:6Da 7:25
Ufu. 13:6Ufu 12:12
Ufu. 13:7Ufu 12:17
Ufu. 13:8Ufu 3:5; 21:27
Ufu. 13:8Isa 53:7; Mt 27:50; Ufu 5:6, 12
Ufu. 13:9Mt 11:15
Ufu. 13:10Mt 26:52
Ufu. 13:10Da 7:18; 1Ko 6:2; Ufu 20:6
Ufu. 13:10Mt 24:13; Ebr 10:36; 12:3
Ufu. 13:10Ufu 2:10
Ufu. 13:11Ufu 16:13; 20:2
Ufu. 13:12Ufu 13:1
Ufu. 13:12Ufu 13:3
Ufu. 13:14Ufu 19:20; 20:4
Ufu. 13:14Ufu 13:3
Ufu. 13:16Ufu 14:9, 10; 16:2; 19:20
Ufu. 13:17Ufu 14:11
Ufu. 13:17Ufu 15:2
Ufu. 13:18Da 3:1
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ufunuo 13:1-18

Ufunuo kwa Yohana

13 Naye* akasimama tuli juu ya mchanga wa bahari.

Nami nikamwona mnyama wa mwituni+ akipanda kutoka baharini,+ naye alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, na mataji kumi* juu ya pembe zake, lakini juu ya vichwa vyake majina yenye makufuru. 2 Basi yule mnyama wa mwituni niliyemwona alikuwa kama chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Na yule joka+ akampa huyo mnyama nguvu zake na kile kiti chake cha ufalme na mamlaka kubwa.+

3 Nikaona kimoja kati ya vichwa vyake kikiwa kimejeruhiwa vibaya lakini jeraha hilo la kifo lilipona,+ na dunia yote ikamfuata kwa mshangao yule mnyama wa mwituni. 4 Nao wakamwabudu yule joka kwa sababu alimpa mamlaka yule mnyama wa mwituni, nao wakamwabudu mnyama wa mwituni kwa maneno haya: “Ni nani aliye kama huyu mnyama wa mwituni, na ni nani anayeweza kupigana naye?” 5 Akapewa kinywa kinachosema mambo makuu na makufuru, akapewa pia mamlaka ya kutenda kwa miezi 42.+ 6 Naye akafungua kinywa chake kwa kumkufuru+ Mungu ili kulikufuru jina lake na makao yake, na hata wale wanaokaa mbinguni.+ 7 Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watakatifu na kuwashinda,+ na akapewa mamlaka juu ya kila kabila na watu na lugha na taifa. 8 Na wale wote wanaokaa duniani watamwabudu. Tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu, hakuna jina la hata mmoja wao lililoandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima+ cha Mwanakondoo aliyechinjwa.+

9 Ikiwa yeyote ana sikio, na asikie.+ 10 Ikiwa yeyote amekusudiwa kwenda utekwani, ataenda utekwani. Ikiwa yeyote ataua* kwa upanga, naye lazima auawe kwa upanga.+ Hapa ndipo watakatifu+ wanahitaji uvumilivu+ na imani.+

11 Kisha nikamwona mnyama mwingine wa mwituni akipanda kutoka katika dunia, naye alikuwa na pembe mbili kama mwanakondoo, lakini akaanza kuzungumza kama joka.+ 12 Anatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza wa mwituni+ aliye machoni pake. Naye huifanya dunia na wale wanaokaa duniani wamwabudu yule mnyama wa kwanza wa mwituni, ambaye jeraha lake la kifo lilipona.+ 13 Naye hufanya ishara kubwa, hata hufanya moto ushuke kutoka mbinguni mpaka duniani machoni pa wanadamu.

14 Naye huwapotosha wale wanaokaa duniani, kwa sababu ya ishara alizoruhusiwa kufanya machoni pa yule mnyama wa mwituni, huku akiwaambia wale wanaokaa duniani watengeneze sanamu+ ya yule mnyama wa mwituni aliyekuwa na pigo la upanga lakini bado akabaki hai.+ 15 Naye akaruhusiwa kuipa pumzi* ile sanamu ya mnyama wa mwituni, ili ile sanamu ya mnyama wa mwituni iweze kusema na pia kufanya wale wote wanaokataa kuiabudu ile sanamu ya mnyama wa mwituni wauawe.

16 Anawalazimisha watu wote—wadogo kwa wakubwa, matajiri kwa maskini, walio huru kwa watumwa—ili wote watiwe alama kwenye mkono wao wa kulia au kwenye paji la uso wao,+ 17 na ili yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama, jina+ la yule mnyama wa mwituni au namba ya jina lake.+ 18 Hapa ndipo hekima inapohitajiwa: Yule aliye na ufahamu na afanye hesabu ya namba ya yule mnyama wa mwituni, kwa maana ni namba ya mwanadamu, na namba yake ni 666.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki