Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waebrania 5
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Waebrania—Yaliyomo

      • Yesu ni mkuu kuliko makuhani wakuu wanadamu (1-10)

        • Kwa mfano wa Melkizedeki (6, 10)

        • Alijifunza utii kutokana na mateso (8)

        • Ana daraka la kuleta wokovu wa milele (9)

      • Onyo dhidi ya kukosa ukomavu (11-14)

Waebrania 5:1

Marejeo

  • +Kut 40:13
  • +Law 5:6

Waebrania 5:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwa wororo; kwa kiasi.”

  • *

    Au “wasiotii.”

  • *

    Au “anakabiliana.”

Waebrania 5:3

Marejeo

  • +Law 9:7; 16:6

Waebrania 5:4

Marejeo

  • +Kut 28:1

Waebrania 5:5

Marejeo

  • +Yoh 8:54
  • +Zb 2:7; Mdo 13:33

Waebrania 5:6

Marejeo

  • +Zb 110:4

Waebrania 5:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Katika siku za mwili wake.”

Marejeo

  • +Lu 22:44; Yoh 12:27

Waebrania 5:8

Marejeo

  • +Mt 26:39; Flp 2:8

Waebrania 5:9

Marejeo

  • +Ebr 7:28
  • +Yoh 3:16

Waebrania 5:10

Marejeo

  • +Zb 110:4

Waebrania 5:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kulingana na wakati.”

Marejeo

  • +Ebr 6:1

Waebrania 5:13

Marejeo

  • +Efe 4:14

Waebrania 5:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nguvu zao za ufahamu.”

Jumla

Ebr. 5:1Kut 40:13
Ebr. 5:1Law 5:6
Ebr. 5:3Law 9:7; 16:6
Ebr. 5:4Kut 28:1
Ebr. 5:5Yoh 8:54
Ebr. 5:5Zb 2:7; Mdo 13:33
Ebr. 5:6Zb 110:4
Ebr. 5:7Lu 22:44; Yoh 12:27
Ebr. 5:8Mt 26:39; Flp 2:8
Ebr. 5:9Ebr 7:28
Ebr. 5:9Yoh 3:16
Ebr. 5:10Zb 110:4
Ebr. 5:12Ebr 6:1
Ebr. 5:13Efe 4:14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Waebrania 5:1-14

Kwa Waebrania

5 Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu huwekwa rasmi kwa ajili yao juu ya mambo yanayohusiana na Mungu,+ ili atoe zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.+ 2 Yeye anaweza kuwatendea kwa huruma* wale wasiojua na wanaokosea,* kwa sababu yeye pia anapambana* na udhaifu wake mwenyewe, 3 na hivyo ni lazima atoe dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe kama vile anavyotoa kwa ajili ya dhambi za watu.+

4 Mtu hapati heshima hii kwa kupenda kwake mwenyewe, bali huipokea tu Mungu anapomwita, kama Haruni alivyoitwa.+ 5 Vivyo hivyo, pia Kristo hakujitukuza mwenyewe+ kwa kuwa kuhani mkuu, bali alitukuzwa na Yule aliyemwambia hivi: “Wewe ni mwanangu; leo nimekuwa baba yako.”+ 6 Kama vile pia anavyosema mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+

7 Alipokuwa duniani,* Kristo alitoa dua na pia maombi, kwa vilio vyenye nguvu na machozi,+ kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumwokoa kutoka katika kifo, naye akasikilizwa vizuri kwa sababu ya kumwogopa Mungu. 8 Ingawa alikuwa mwana, alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata.+ 9 Na baada ya kufanywa kuwa mkamilifu,+ akawa na daraka la wokovu wa milele kwa ajili ya wote wanaomtii,+ 10 kwa sababu Mungu amemteua kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.+

11 Tuna mengi ya kusema kumhusu na ni vigumu kuyafafanua, kwa sababu mmekuwa wazito wa kusikia. 12 Kwa maana, ingawa kufikia sasa* mnapaswa kuwa walimu, mnahitaji tena mtu awafundishe tangu mwanzo mambo ya msingi+ ya maneno matakatifu ya Mungu, nanyi mnahitaji maziwa tena, bali si chakula kigumu. 13 Kwa kuwa kila mtu anayeendelea kunywa maziwa hafahamu neno la uadilifu, kwa maana yeye ni mtoto mdogo.+ 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wakomavu, ambao wamezoeza nguvu zao za utambuzi* kwa kuzitumia ili kutofautisha mambo yaliyo sawa na mambo yasiyo sawa.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki