Zaburi
94 Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+
Ee Mungu wa kisasi, angaza!
2 Inuka, Ee Mwamuzi wa dunia.+
Walipe wanachostahili watu wenye kiburi.+
3 Waovu wataendelea mpaka lini, Ee Yehova,
Waovu wataendelea mpaka lini kushangilia?+
4 Wanaropoka na kuongea kwa kiburi;
Watenda dhambi wote wanajigamba kujihusu.
5 Wanawaponda watu wako, Ee Yehova,+
Na kuukandamiza urithi wako.
6 Wanamuua mjane na mkaaji mgeni,
Na kuwaua mayatima.
8 Eleweni jambo hili, ninyi msiotumia akili;
Ninyi wajinga, ni lini mtakapoonyesha ufahamu?+
9 Yule aliyetengeneza* sikio, je, hawezi kusikia?
Yule aliyeumba jicho, je, hawezi kuona?+
10 Yule anayeyarekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+
Yeye Ndiye anayewafundisha watu ujuzi!+
11 Yehova anajua mawazo ya wanadamu,
Ya kwamba ni pumzi tu.+
12 Mwenye furaha ni mtu unayemrekebisha, Ee Yah,+
Unayemfundisha kwa sheria yako,+
13 Ili kumpa utulivu katika siku za msiba,
Mpaka shimo litakapochimbwa kwa ajili ya mwovu.+
15 Kwa maana kwa mara nyingine tena hukumu itakuwa ya uadilifu,
Na wote walio wanyoofu moyoni wataifuata.
16 Ni nani atakayeinuka dhidi ya waovu kwa ajili yangu?
Ni nani atakayenitetea dhidi ya watenda maovu?
18 Niliposema: “Mguu wangu unateleza,”
Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+
20 Je, kiti cha ufalme* chenye ufisadi kinaweza kuungana nawe
23 Atafanya matendo yao maovu yawarudie.+
Atawaangamiza* kwa uovu wao wenyewe.