Zaburi
Kwa kiongozi; mtindo wa Yeduthuni.* Muziki wa Asafu.+
77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu;
Nitamlilia Mungu kwa sauti kubwa, naye atanisikia.+
2 Katika siku ya taabu yangu ninamtafuta Yehova.+
Usiku ninamnyooshea mikono yangu bila kuacha.*
Siwezi* kufarijiwa.
4 Unazishika kope zangu ili nisifumbe macho;
Nimefadhaika, nami siwezi kuongea.
5 Mawazo yangu yanarudi katika siku za zamani za kale,+
Miaka mingi iliyopita.
7 Je, Yehova atatutupa mbali milele?+
Je, hatatuonyesha tena kamwe kibali chake?+
8 Je, upendo wake mshikamanifu utakoma milele?
Je, ahadi yake itakosa kutimia katika vizazi vyote?
9 Je, Mungu amesahau kuonyesha kibali chake,+
Au je, hasira yake imekomesha rehema yake? (Sela)
10 Je, ni lazima niendelee kusema: “Hili ndilo linalonitaabisha:*+
Aliye Juu Zaidi amebadili msimamo wake kutuelekea”?*
11 Nitazikumbuka kazi za Yah;
Nitayakumbuka matendo yako yanayostaajabisha ya zamani za kale.
12 Nitautafakari utendaji wako wote
Na kutafakari shughuli zako.+
13 Ee Mungu, njia zako ni takatifu.
Ee Mungu, ni mungu gani aliye mkuu kama wewe?+
14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayetenda mambo yanayostaajabisha.+
Umeyafunulia mataifa nguvu zako.+
16 Maji yalikuona, Ee Mungu,
Maji yalikuona yakavurugika.+
Na vilindi vya maji vikatibuka.
17 Mawingu yakamwaga maji.
Anga lenye mawingu likanguruma,
Na mishale yako ikaruka huku na kule.+
18 Sauti ya mngurumo+ wako ilikuwa kama magurudumu ya gari la vita;
Mimweko ya radi iliangaza dunia inayokaliwa;*+
Dunia ilitikisika na kutetemeka.+
19 Njia yako ilipita baharini,+
Kijia chako kilipita katika maji mengi;
Lakini nyayo zako hazingeweza kuonekana.