Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yakobo 5
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yakobo—Yaliyomo

      • Onyo kwa matajiri (1-6)

      • Mungu huwabariki wanaovumilia kwa subira (7-11)

      • Acheni “ndiyo” yenu iwe ndiyo (12)

      • Sala ya imani ina nguvu (13-18)

      • Kumsaidia mtenda dhambi arudi (19, 20)

Yakobo 5:1

Marejeo

  • +Met 11:28; Lu 6:24; 18:25

Yakobo 5:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina ya wadudu.

Marejeo

  • +Mt 6:19; Lu 12:33

Yakobo 5:3

Marejeo

  • +Eze 7:19

Yakobo 5:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Law 19:13; Kum 24:14, 15; Yer 22:13; Mal 3:5

Yakobo 5:5

Marejeo

  • +Yer 12:3

Yakobo 5:7

Marejeo

  • +Mt 24:3
  • +Kum 11:14; Yer 5:24

Yakobo 5:8

Marejeo

  • +Ebr 6:12
  • +1Th 3:13

Yakobo 5:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Msizomeane; Msilalamikiane.”

Marejeo

  • +1Ko 4:5

Yakobo 5:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Mt 5:12
  • +Ebr 6:12
  • +2Nya 36:16

Yakobo 5:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wamebarikiwa.”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

  • *

    Au “ni mwenye huruma sana.”

Marejeo

  • +Yak 1:2-4
  • +Ayu 1:20, 21
  • +Ayu 42:10
  • +Zb 103:8; Lu 6:36

Yakobo 5:12

Marejeo

  • +Mt 5:34-37

Yakobo 5:13

Marejeo

  • +Zb 50:15
  • +Kol 3:16

Yakobo 5:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Mdo 20:28, 35; 1Pe 5:2
  • +Zb 141:5; Mk 6:13; Lu 10:34

Yakobo 5:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “aliyechoka.”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Yakobo 5:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ina nguvu nyingi inapofanya kazi.”

Marejeo

  • +2Sa 12:13; Zb 32:5; Met 28:13; 1Yo 1:9
  • +1Sa 12:18; 1Fa 13:6

Yakobo 5:17

Marejeo

  • +1Fa 17:1

Yakobo 5:18

Marejeo

  • +1Fa 18:42, 45

Yakobo 5:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ataokoa nafsi yake.”

Marejeo

  • +Gal 6:1
  • +1Ti 4:16

Jumla

Yak. 5:1Met 11:28; Lu 6:24; 18:25
Yak. 5:2Mt 6:19; Lu 12:33
Yak. 5:3Eze 7:19
Yak. 5:4Law 19:13; Kum 24:14, 15; Yer 22:13; Mal 3:5
Yak. 5:5Yer 12:3
Yak. 5:7Mt 24:3
Yak. 5:7Kum 11:14; Yer 5:24
Yak. 5:8Ebr 6:12
Yak. 5:81Th 3:13
Yak. 5:91Ko 4:5
Yak. 5:10Mt 5:12
Yak. 5:10Ebr 6:12
Yak. 5:102Nya 36:16
Yak. 5:11Yak 1:2-4
Yak. 5:11Ayu 1:20, 21
Yak. 5:11Ayu 42:10
Yak. 5:11Zb 103:8; Lu 6:36
Yak. 5:12Mt 5:34-37
Yak. 5:13Zb 50:15
Yak. 5:13Kol 3:16
Yak. 5:14Mdo 20:28, 35; 1Pe 5:2
Yak. 5:14Zb 141:5; Mk 6:13; Lu 10:34
Yak. 5:162Sa 12:13; Zb 32:5; Met 28:13; 1Yo 1:9
Yak. 5:161Sa 12:18; 1Fa 13:6
Yak. 5:171Fa 17:1
Yak. 5:181Fa 18:42, 45
Yak. 5:20Gal 6:1
Yak. 5:201Ti 4:16
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yakobo 5:1-20

Barua ya Yakobo

5 Haya basi, enyi matajiri, lieni na kupiga mayowe kwa sababu ya taabu zitakazowapata.+ 2 Utajiri wenu umeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.*+ 3 Dhahabu na fedha zenu zimeliwa na kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu nayo itakula miili yenu. Vitu mlivyoweka akiba vitakuwa kama moto katika siku za mwisho.+ 4 Tazama! Mishahara ambayo hamjawalipa wafanyakazi waliovuna mashamba yenu, inaendelea kupaza kilio, na vilio vya kuomba msaada vya wavunaji vimefika masikioni mwa Yehova* wa majeshi.+ 5 Ninyi mmeishi kwa anasa na kwa ajili ya kutosheleza tamaa zenu duniani. Mmeinonesha mioyo yenu katika siku ya machinjo.+ 6 Mmemhukumu; mmemuua mwadilifu. Je, yeye hawapingi ninyi?

7 Basi, iweni na subira, akina ndugu, mpaka kuwapo kwa Bwana.+ Tazama! Mkulima huendelea kungojea matunda yenye thamani ya nchi, akiyasubiri mpaka mvua ya mapema na mvua ya baadaye inyeshe.+ 8 Ninyi pia iweni na subira;+ imarisheni mioyo yenu, kwa sababu kuwapo kwa Bwana kumekaribia.+

9 Msinung’unikiane,* akina ndugu, ili msihukumiwe.+ Tazama! Mwamuzi amesimama mbele ya milango. 10 Akina ndugu, fuateni mfano wa manabii waliopatwa na uovu+ na kuonyesha subira+ na ambao walisema katika jina la Yehova.*+ 11 Tazama! Tunawaona wale ambao wamevumilia kuwa wenye furaha.*+ Mmesikia kuhusu uvumilivu wa Ayubu+ na mmeona matokeo ambayo Yehova* alileta,+ kwamba Yehova* ni mwenye upendo mwororo sana* na mwenye rehema.+

12 Zaidi ya yote, akina ndugu, acheni kuapa kwa mbingu au kwa dunia au kwa kiapo kingine chochote. Bali acheni “Ndiyo” yenu iwe ndiyo, na “Siyo” yenu, siyo,+ ili msihukumiwe.

13 Je, kuna yeyote kati yenu aliye na matatizo? Na aendelee kusali.+ Je, kuna yeyote mwenye roho changamfu? Na aimbe zaburi.+ 14 Je, kuna yeyote aliye mgonjwa kati yenu? Na awaite wazee+ wa kutaniko, nao wasali kwa ajili yake, wakimpaka mafuta+ katika jina la Yehova.* 15 Na sala ya imani itamponya huyo mgonjwa,* na Yehova* atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.

16 Kwa hiyo ungameni waziwazi dhambi zenu+ kwa mtu na mwenzake na kusali kwa ajili ya mtu na mwenzake, ili mponywe. Dua ya mtu mwadilifu ina nguvu nyingi.*+ 17 Eliya alikuwa mtu mwenye hisia kama zetu, na bado aliposali kwa bidii mvua isinyeshe, haikunyesha juu ya nchi kwa miaka mitatu na miezi sita.+ 18 Naye akasali tena, na mbingu ikatoa mvua na nchi ikazaa matunda.+

19 Ndugu zangu, yeyote kati yenu akipotoshwa kutoka katika kweli na mwingine amrudishe, 20 jueni kwamba yeyote anayemrudisha mtenda dhambi kutoka kwenye kosa+ la njia yake atamwokoa* kutoka kwenye kifo naye atafunika dhambi nyingi.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki